NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amefanya ziara ya Siku mbili katika mikoa ya Shinyanga na Geita na kukagua miradi mbalimbali. 

Akiwa Mkoani Shinyanga, Jafo alitembelea Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambapo alijionea changamoto mbali mbali ikiwepo ya Jengo dogo linalotumiwa na kinamama wakati wakujifungua kutokana na hospitali hiyo kuzidiwa uwezo.

Kufuatia hali hiyo, Jafo amemuagiza Injinia wa Wilaya kuhakikisha wanaharakisha ujenzi wa Jengo kubwa la kisasa la kinamama kwani fedha zipo za Ujenzi huo ili wagonjwa wasiendelee kupata mateso kwa michakato ya Ujenzi mirefu isiyo na tija.

Kadhalika, akiwa wilayani Kahama, Naibu Waziri Jafo ametembelea Mradi wa Soko na kumuagiza Mkurugenzi wa Wilaya, Andason Msumba, kuhakikisha anakaa na timu yake ya Wataalamu ili kutatua mgogoro wa Soko hilo kwa Maslahi mapana ya wananchi wa Mji wa Kahama.

Amehitimisha Ziara yake mkoani Shinyanga kwa kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama na Halmashauri ya Msalala ambapo amewataka Watumishi kufanya kazi kwa kujituma huku wakiepuka Uzembe kazini,upendeleo, kupigana majungu, na kuchukiana.

Katika mkoa wa Geita, Jafo amekagua mradi wa Maji na Kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti wilayani Chato huku akimuagiza Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo kuhakikisha mradi unakamilika mapema kabla ya Mwezi wa 10 ili kuweza kusaidia kutatua changamoto ya Maji.

Amesema wananchi hawawezi kuwa na Upungufu wa Maji wakati kuna maji mengi ya Ziwa Victoria. Akikagua Mradi wa kiwanda cha kukamua Mafuta ya Alizeti, Jafo alimwagiza Mkurugenzi kuhakikisha anashirikiana na Sido ili kuweza kuukamilisha mradi huo haraka.

Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akizungumza na wananchi nje ya kiwanda cha kukamulia alizeti mjini Chato.
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mashine za kukamulia mafuta ya alizeti mjini Chato.
Mkurugenzi wa mji wa Kahama, Andason Msumba akitoa maelezo kwa Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo kuhusu mgogoro wa soko  wanalolitaka wananchi kutumika kwa maslahi ya wananchi wa mji huo. 
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mradi wa maji  kijiji cha Chankorongo wilayani Geita uliohujumiwa na watendaji na kumuagiza Katibu tawala wa mkoa wa Geita kuunda timu ya uchunguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...