Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na ambaye sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dr. Modestus Kipilimba leo amekabidhi rasmi ofisi kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu mpya Bw. Andrew Wilson Massawe; aliyeteuliwa hivi karibu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA. 
Katika Hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA, Dr. Modestus Kipilimba amekabidhi ripoti yenye mjumuisho wa taarifa ya utekelezaji mradi wa Vitambulisho vya Taifa na hatua za utekelezaji. 
Halfa hiyo ilifuatiwa na ziara fupi ya kutembelea kituo cha uchakataji taarifa na uzalishaji vitambulisho (Data Centre) ambapo mbali na kukagua shughuli za uzalishaji, Bw. Massawe alipata fursa ya kukagua mitambo na ubora wa vitambulisho vinavyozalishwa.
 Dr. Modestus Kipilimba (Kushoto) akimkabidhi ripoti ya utekelezaji mradi wa vitambulisho vya Taifa Bw. Andrew Wilson Massawe aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA wakati wa hafla ya Makabidhiano katika ofisi za  Makao makuu ya NIDA jijini Dar es salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. Andrew Wilson Massawe akizungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa mara baada ya hafla ya makabidhiano

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, Bw. Andrew Wilson Massawe akikagua mitambo ya uzalishaji vitambulisho alipotembea kituo cha uchakataji na uzalishaji vitambulisho mara baada ya halfa ya makabidhiano. Kulia ni   Dr. Modestus Kipilimba

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA, akikagua mfumo wa uhifadhi taarifa wakati alipotembelea kituo cha uchakataji taarifa (Data Centre) na kushuhudia mfumo wa kielektroniki unavyoendesha shughuli mbalimbali za uzalishaji na uhifadhi wa taarifa katika kituo hicho
 Dr. Modestus Kipilimba (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bw. Andrew Wilson Massawe wakiwa katika  picha ya pamoja na Menejimenti ya NIDA, baada ya hafla fupi ya makabidhiano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...