Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara(TanTrade) Bw Edwin Rutageruka akipata naelezo kutoka kwa Bw John Julius juu ya uzalishaji wa mafuta ya ufuta katika banda la halmashauri ya Masasi kwenye maonesho ya 88 mkoani Lindi. Mafuta ya ufuta yanasoko kubwa sana nje ya Afrika hasa nchi ya Japan na ni mafuta ya pili yenye ubora baada ya olive oil. 
Lengo kuu tasisi hii kushiriki maonesho haya ni kuunganisha wazalishaji na masoko ya ndani na nje ya nchi. Hivo imekuwa ikipita kwa wazalishaji mbalimbali kuangalia fursa za kuwaungaisha na masoko mbalimbali ili kukuza uchumi wa nchi yetu na pia kualika wawekezaji katika nchi yetu na kuifanya Tanzania yenye viwanda. Tantrade imeshirik katika maonesho haya maarufu kama 88 kwenye kanda tano ambazo ni Lindi, Morogoro, Mwanza, Mbeya na Arusha na kila mkoa wazalishaji hutofautiana kutokana na aina za uzalishaji wa bidhaa za kila mkoa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...