Kampuni ya State Grid ya China imeonesha nia ya kuwekeza katika Mradi wa Kujenga Njia ya umeme ya Msongo wa kV 400 ya kutoka Mchuchuma hadi Makambako.

Hayo yamebainika katika kikao kati ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Balozi wa China nchini, Dkt Lu Youqing aliyeambatana na ujumbe huo wa kampuni hiyo.

Profesa Muhongo alichukua fursa hiyo kuieleza kampuni hiyo kuhusu Hazina iliyopo nchini ya Makaa ya Mawe na kusema kuwa, bado Serikali inatafuta wawekezaji ambao watazalisha umeme kwa kutumia chanzo hicho na kuongeza kuwa, “Bado tunahitaji wawekezaji kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe”.

Aidha, mbali na kuonesha nia ya kuwekeza katika Mradi huo, Kampuni hiyo imefika Wizarani kutaka kujua maeneo mengine ya uwekezaji katika sekta ya Nishati ambayo kampuni hiyo inaweza kufanya kazi nchini.

Vilevile, kampuni hiyo ilimweleza Waziri uzoefu ilionao katika shughuli hizo na kuzitaja baadhi ya nchi ambazo inatekeleza miradi kama hiyo kuwa barani Afrika kuwa ni pamoja na Ethiopia, Egypt, Kenya na Afrika Kusini.
Waziri wa Nishati na Madini (katikati) Profesa Sospeter Muhongo akiwaeleza jambo Balozi wa China nchini, Dkt. Lu Youqing (wa kwanza kushoto) na ujumbe wake waliofika Ofisini kwa Waziri ili kufahamu namna kampuni hiyo inavyoweza kufanya kazi katika sekta ya Nishati nchini.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akieleza jambo wakati wa kikao baina yake na Balozi wa China nchini, Dkt. Lu Youqing (wa kwanza kushoto) na ujumbe wake waliofika Ofisini kwa Waziri ili kufahamu namna kampuni ya State Grid ya China inavyoweza kufanya kazi katika sekta ya Nishati nchini.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akimsikiliza Mwakilishi wa Kampuni ya State Grid ya China upande wa Afrika, Mingu Liu, (wa kwanza kulia mbele) wakati akimweleza Waziri Muhongo azma ya Kampuni hiyo kuwekeza katika Mradi wa Ujenzi wa Njia ya Umeme ya Msongo wa kV 400 Mchuchuma hadi Makambako. Wengine wanaofuatilia ni Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing na ujumbe wake.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiangalia Makabrasha kutoka Kampuni ya State Grid ya China ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika mradi wa ujenzi wa njia ya umeme ya Msongo wa kV 400 ya Mchuchuma hadi Makambako.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikakti) na Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youging (wa pili kushoto) na ujumbe wake wakifurahia jambo mara baada ya kumalizika kwa kikao baina ya Waziri, Balozi na kampuni ya State Grid.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...