Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...