MKURUGENZI wa Halmashauri ya wilaya
ya Namtumbo Bw. Christopher Kilungu (kushoto) akiongoza baraza la
madiwani kulipitia kabrasha la kikao hicho.
Kikao hicho cha baraza
la madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kilimkataa kaimu
Katibu wa Tume ya Utumishi wa walimu (TSC) Boniphace Fungo na kutoa
onyo kwa watumishi wawili - Mkuu wa idara ya kilimo Ally Lugendo na mkuu wa
idara ya Ujenzi David Mwanapemba - na pia kilimuagiza Mkurugenzi wa
Halmashauri hiyo kuwachukulia hatua ya kinidhamu Mkuu wa idara ya
fedha Clodwick Mapunda na Mkuu wa idara ya Manunuzi kwa utendaji
usioridhisha kwenye idara zao
Kikao cha baraza la madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kikiendelea
Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo wakiwa kwenye kikao cha baraza
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...