Mmoja wa wacehezaji wa timu ya Lugalo Golf Club,Nicholaus Chitanda akionesha makombe waliyoyanyakuwa mara baada ya timu yao kuibuka washindi wa mashindano ya Golf yaliyojulikana kwa jina la MOSHI OPEN,yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.Timu hiyo ya golf ya Jeshi ya Lugalo imewapa raha wanachama wake akiwemo Mlezi wa Klabu hiyo ambaye ni Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange kwa kurejesha Ubingwa wa mashindano ya MOSHI OPEN.Timu hiyo ya Golf  imeirejesha heshima yake kwa wanachama na wapenzi wake kwa kuibuka na vikombe,ambapo mara ya mwisho klabu hiyo kuibuka na ushindi ilikuwa ni mwaka 2014.
Timu ya Lugalo Golf Club wakiwa katika picha ya pamoja mara baada
ya kuibuka washindi wa mashindano ya Golf yaliyojulikana kwa jina la MOSHI OPEN,yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki,Mashindano hayo yalizishirikisha timu ya Ghymkana,timu ya Golf Moshi pamoja na timu ya Gofu ya jijini Arusha.
Mmoja wa washiriki wa timu ya Lugalo Golf Club Noel Mheni akiwa mwenye furaha mara baada ya kuibuka washindi wa mashindano ya Golf yaliyojulikana kwa jina la MOSHI OPEN,yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.Timu hiyo ya golf ya Jeshi ya Lugalo imewapa raha wanachama wake akiwemo Mlezi wa Klabu hiyo ambaye ni Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange kwa kurejesha Ubingwa wa mashindano ya Moshi Open .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...