Balozi wa
Uganda nchini Tanzania Bi. Dorothy Samali Hyuha akisaini kitabu cha maombolezo
na kutoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekua Rais wa Pili wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
Mwakilishi
wa Ubalozi wa Nigeria nchini Bi. Abiola Sherif Deluya akitoa salamu za pole
katika kitabu maalumu kilichopo katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa Luthuli,
Jijini Dar es Salaam leo.
Balozi wa Palestina Mheshimiwa
Hazim Shabat ni miongoni mwa mabalozi waliotembelea Ofisi ya Makamu wa Rais leo na
kutoa salamu za pole kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa
Zanzibar.
Balozi wa
Kuwait nchini Tanzania Bw. Jassem Al
Najem ni miongoni mwa mabalozi waliotembelea Ofisi ya Makamu wa Rais leo na
kutoa salamu za pole kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa
Zanzibar. Picha zote
na Ofisi ya Makamu wa Rais
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...