Madiwani wa kimsikiliza Kwa makini Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega katika kikao cha halmashauri ya wilaya ya Mkuranga.Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga Kwa kauli moja wamepitisha maadhimio ya kuunda kamati itakayokwenda Kwa Waziri Mkuu ili kumuomba rais afute hati miliki ya shamba namba 271, linalomilikiwa na mwekezaji, Hamidu Balma. 
 
Shamba hilo ambalo lenye hekari 1750 ambalo lipo katika kata ya Mwandege limeingia katika mgogoro mkubwa na wananchi wa kijiji cha kazole, hadi kufikia hatua ya wananchi hao kulala mahabusu Mara kadhaa kwasababu ya wanakijiji hao kuingia katika shamba hilo ambalo limekaa zaidi ya miaka 28 bila kuendelezwa.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya hiyo, katika kikao chao madiwani ,ambapo katika kikao hicho waliadhimia kwa kauli moja kumuomba Rais kufuta hati miliki ya shamba la Soap and Allied industries limited ambalo linamilikiwa na Hamidu Balma lililopo mkoani Pwani kwa kushindwa kuliendeleza.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga,filbarto Sanga akizungumza katika mkutano wa baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya ya Mkuranga ,ambapo kikubwa alizungumzia suala la uimarishaji wa ulinzi na usalama ndani ya wilaya hiyo,kulia ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga Juma Abeid (alie simama) akizungumza katika kikao hicho cha baraza la madiwani lililofanyika jana

Diwani wa Kata ya Mwandege Adolph Edward akichangia hoja katika kikao hicho cha Baraza la madiwani katika Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo ziliibuka hoja mbalimbali ikiwamo ya mwekezaji Hamidu Balma aliyeshindwa kuendeleza shamba namba 271,lililopo katika kataka ya Mwandege

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...