Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia sekta ya Mawasiliano Dkt. Maria Sasabo akitoa maelezo ya kituo mahiri cha kutunza kumbukumbu (internet Data Centre) kwa Makatibu Wakuu hawapo pichani walipotembelea kituo hicho kilichopo eneo la Kijitonyama DSM.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Dkt. Yamungu Kayandabila katikati akitoa maoni yake kuhusu kituo mahiri cha kutunza kumbukumbu “ internet Data Centre”, (wa kwanza kulia) ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya nje na Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi na (wa kwanza kushoto) ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bibi Florence Mwanri walipokitembelea kituo hicho eneo la Kijitonyama DSM. Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...