Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na Wakuu wa Taasisi za Umma za Fedha Zanzibar Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d. 
Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d akimueleza Balozi Mikakati inayochukuliwa na Wizara yake katika suala zima la ukusanyaji wa Mapato ya Serikali.
Picha na –OMPR – ZNZ.

Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar { ZRB }, Ndugu Hamil Bakar  alisema kwamba makusanyo ya Mapato kwa mwezi wa Juni mwaka huu yamefikia shilingi Bilioni Kumi na Sita ikikadiriwa kufikia lengo la makusanyo ya shilingi Bilioni Ishirini mwezi Julai mwaka huu.

Hata hivyo alisema yapo baadhi ya makusanyo yanayofikia shilingi Bilioni Mbili ambayo hupatikana kutokana na mapato ya Wizara na Taasisi mbali mbali za Umma.

Kamishna Hamil  alitoa takwimu hizo katika kikao cha pamoja kati ya Watendaji Wakuu wa Taasisi za Fedha wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d walipokutana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Balozi Seif ameitisha Kikao hicho ikiwa ni muendelezo wa Mikutano yake ya kukutana na watendaji wapya wa Taasisi hizo kwa kutambuana kufuatia mabadiliko ya muundo mpya wa Serikali sambamba na kuangalia fursa za kukabiliana na changamoto zinazozikabili Taasisi hizo.

Akitoa taarifa fupi katika Kikao hicho Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d alieleza kwamba Bodi ya Mapato Zanzibar ilipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni Mia 272 kwa mwaka kati ya hizo shilingi Bilioni 35.2 zinatokana na mapato ya Wizara.

Dr. Khalid alisema Miezi ya Aprili, Mei na Juni Mwaka huu makusanyo ya mapato yalikadiriwa  kufikia shilingi Bilioni 117 ambapo mwezi juni pekee  makusanyo ya mapato yalifikia  shilingi Bilini 49 ikilinganishwa na mapato ya shilingi Bilioni 37 ya nyuma yake.

Waziri Khalid alimthibitishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba ukusanyaji wa mapato kwa sasa unakwenda  vizuri na kutoa fursa njema ya kupatikana kwa wakati mishahara ya wafanyakazi wa Taasisi za Umma pamoja na viinua Mgongo vya watumishi waliostaafu.

Dr. Khalid alifafanua kwamba watumishi wa umma waliostaafu kazi tokea mwaka 2015 kwa mujibu wa sheria na kanuni za Utumishi  Serikalini tayari wameshapata viinua mgongo vyao.

Alisema watumishi wastaafu wanaoendelea kusubiri haki yao kwa sasa ni wale waliostaafu katika kipindi cha miezi sita ndani ya mwaka huu wa 2016.

Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar { PBZ } Ndugu Juma Ameir Hafidh alisema utendaji wa Taasisi hiyo uko katika kiwango   kinachokubalika kibiashara kutokana na ushirikiano mzuri na Mabenki mengine hapa Nchini.

Hata hivyo ndugu Juma alisema zipo changamoto zinazoikabili Benki hiyo ikiwa ni pamoja na usumbufu wa kuchelewa kwa kesi zake dhidi ya Wateja wanaochukuwa Mikopo kwa ajili ya uwekezaji wa miradi tofauti nchini.

Alisema Mwekezaji asiye na mtaji mara nyingi husababisha mitihani katika kuanzisha miradi ambayo baadaye hukumbwa na ukosefu wa fedha za kurejesha deni alilokopeshwa.
Mkurugenzi Mtendaji huyo wa Benki ya Watu wa Zanzibar aliiomba Serikali Kuu kupitia Taasisi na vitengo vinavyohusika na masuala ya uwekezaji kuhakikisha kwamba vinaratibu kwa kina viwango vya fedha za mitaji  vinavyomlazimisha Mwekezaji kuanzisha mradi utakaompa uwezo wa kuchukuwa mkopo.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
03/08/2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...