Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema (wa pili kushoto), akitoa ufafanuzi hii leo Jijini Mwanza kuhusiana na Maonesho ya Wafanyabiashara Afrika Mashariki yanayotarajiwa kuanza Agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viwanja vya Rock City Jijini Mwanza.


Wengine ni, Hassan Karambi ambaye ni Katibu Mtendaji wa TCCIA Mwanza (wa kwanza kushoto), Tungu Misululu, Makamu Mwenyekiti TCCIA kitengo cha Biashara mkoani Mwanza (wa pili kulia) na Majid Igangula (wa kwanza kulia), kutoka bodi ya Washauri TCCIA.

Makampuni pamoja na wajasiriamali mbalimbali katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania, yametakiwa kutumia Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki katika kutangaza na kuuza bidhaa zao.

Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema, ametoa rai hiyo leo Jijini Mwanza, wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na Maonesho hayo.

"Maonesho haya yanatoa fursa kwa makampuni mbalimbali Afrika Mashariki kujitangaza, kukutana na wateja wao, kutafuta wabia wapya wa kibiashara pamoja na kufanya utafiti wa kimasoko". Ametanabaisha Lema.

Maonesho hayo yanatarajiwa kuanza agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viunga vya Rock City Mall Jijini Mwanza na yanatarajiwa kushirikisha wafanyabiashara kutoka mataifa ya Afrika Mashariki na nje ya Afrika Mashariki.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema (katikati), akiwa katika mkutano na wanahabari (hawapo pichani) kuhusiana na Maonesho ya Wafanyabiashara Afrika Mashariki yanayotarajiwa kuanza Agost 26,2016 hadi Septemba 04,2016 katika viwanja vya Rock City Jijini Mwanza.

Wengine ni, Hassan Karambi ambaye ni Katibu Mtendaji wa TCCIA Mwanza (kushoto), Tungu Misululu, Makamu Mwenyekiti TCCIA kitengo cha Biashara mkoani Mwanza (kulia).
Wanahabari Jijini Mwanza, wakiwa katika Mkutano wa TCCIA kuhusu Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki Jijini Mwanza, uliofanyika leo.
Wanahabari wakiwa katika mkutano huo
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA mkoani Mwanza, Leopard Lema, akitoa ufafanuzi kwa wanahabari.
Taswira ya Mkutano wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo TCCIA, na Wanahabari ulioketi hii leo Jijini Mwanza, kuhusu Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashari yanayotarajiwa kuanza Agost 26 mwaka huu viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza.

Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @BMG

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...