Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wa pili kulia),
akishirikiana na viongozi wengine akiwemo Mbunge wa Jimbo la Segerea,Mheshimiwa Bonnah
Kaluwa(wa kwanza kushoto),kuzindua ujenzi wa kituo cha polisi kinachojengwa katika Jimbo la
Segerea ikiwa ni mkakati wa kupambana na uhalifu katika jimbo hilo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akishiriki ujenzi
wa awali wa kituo cha polisi kinachojengwa katika Jimbo la Segerea ikiwa ni mkakati wa Mbunge wa
jimbo hilo kupambana na vitendo ya uhalifu katika jimbo hilo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(suti nyeusi),
akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya Ujenzi wa Kituo cha Polisi .Naibu
Waziri huyo pia aliongoza Harambee ya Ujenzi wa kituo hicho ikiwa ni mkakati wa Mbunge wa
Jimbo hilo Bonnah Kaluwa, kupambana na matukio ya uhalifu.Naibu Waziri huyo aliongoza.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza
wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kituo cha Polisi .Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la
Segerea,Mheshimiwa Bonnah Kaluwa. Ujenzi wa kituo hicho ni mkakati wa kupambana na matukio
ya uhalifu yanayotokea katika jimbo hilo.
Mbunge wa Jimbo la Segerea la Segerea, Bonnah Kaluwa, akimuongoza Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(suti nyeusi) na viongozi wengine kwenda kutembelea eneo
ambapo ujenzi wa kituo cha polisi katika jimbo hilo umeanza ikiwa ni mkakati wa kupambana na
matukio ya uhalifu jimboni hapo.
Wananchi wa Jimbo la Segerea, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kituo cha Polisi
ikiwa ni mkakati wa Mbunge wa Jimbo hilo, Bonnah Kaluwa, kupambana na matukio ya uhalifu
katika jimbo hilo.(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...