Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye akipokea maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi, jana katika banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwenye maonesho ya Nanenane Kitaifa mkoani Lindi, kabla ya kufungwa na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Bi. Fatma Matimba (kulia) akitoa maelezo kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lindi, juu ya ufanyaji wa kazi wa kifaa cha ukaguzi wa abiria kabla ya kuingia eneo la kwenda kupanda ndege, walipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), katika maonesho ya Nanenane kitaifa Lindi.
Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Geofrey Zambi (wa kwanza kulia) akipokea maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhandisi Diana Munubi (wa pili kushoto), wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwenye maonesho ya Nanenane mkoani Lindi, ambapo yalifikia kilele jana na kufungwa na Mhe. Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...