Mbunge
wa
Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akiwa na baadhi viongozi wa vijiji
wakielekea eneo lengine kukutana na wananchi na kuyasikiliza na kutatua
matatizo yao kwa namna moja ama nyingine wilayani Mkuranga,mkoa wa Pwani
Mbunge Abdallah Ulega akijionea hali halisi ya miundombinu ya usafiri kwa wananchi wake wa Mkuranga mkoani Pwani
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kurutu kilichopo kata shungubweni wilayani Mkuranga katika ziara zake za kushukuru wanakijiji hao Kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
Shabani Omary akiuliza swali kwa mbunge wa jimbo la mkuranga Abdallah Ulega leo mkoani Pwani
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na walimu wa shule ya msingi kijiji cha Kurutu kilichopo kata ya shungubweni leo mkoani Pwani.
wananchi wa kijiji cha Kurutu kilichopo kata shungubweni wilayani Mkuranga wameshauliwa kuchukua shamba lenye ukubwa wa hekari 66.6 ambalo alipewa mwekezaji Salim tangu mwaka 1988 na kushindwa kuliendeleza,ili walitumie Kwa shughuli za kuzalisha mali.
Ushauri huo ulitolewa wilayani humo na Mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega mara baada ya kupokea malalamiko Kutoka Kwa wananchi wake akiwa katika ziara zake za kushukuru wanakijiji hao Kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
Ulega alisema haiwezikani watu wanajimilikisha mashamba makubwa miaka hadi miaka alafu wanashindwa kuyaendelea huku wananchi wakipata shida ya kukosa maeneo hata ya kulima kilimo cha mbogamboga vijana.
"Nasema kuwa kama shamba hilo limekaa miaka yote hiyo haliendelezwi, napia huyo mwekezaji haonikani sasa mnasubiri nini kulichukua na kufanya uendelezaji,nashauri litwaeni alafu tutapambana nayo huko mbele"
Pia Ulega aliwaeleza wananchi hao kuwa siasa imekwisha na kilichobaki ni watu kufanya Kazi Kwa nguvu zote na kwamba atakuwa bega Kwa bega katika kuhakikisha maendeleo wanayapata Kwa haraka.
Awali wananchi wa kijini cha Kurutu walimweleza mbunge kuwa wanashamba kubwa ambalo alipewa mwekezaji miaka mingi iliyopita tena kienyeji lakini hadi leo ameshindwa kuliendeleza hivyo awasaidie walipate ili vijana wa eneo hilo wazalishe chumvi.
Mbunge huyo bado anaendelea na ziara zake za kutembelea kijiji hadi kijiji kwa lengo la kuwashukuru na kuhimiza shughuli za maendeleo ambapo anawataka kujituma katika kufanya kazi kwani wilaya hiyo imechelewa kimaendeleo.
Shabani Omary akiuliza swali kwa mbunge wa jimbo la mkuranga Abdallah Ulega leo mkoani Pwani
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na walimu wa shule ya msingi kijiji cha Kurutu kilichopo kata ya shungubweni leo mkoani Pwani.
wananchi wa kijiji cha Kurutu kilichopo kata shungubweni wilayani Mkuranga wameshauliwa kuchukua shamba lenye ukubwa wa hekari 66.6 ambalo alipewa mwekezaji Salim tangu mwaka 1988 na kushindwa kuliendeleza,ili walitumie Kwa shughuli za kuzalisha mali.
Ushauri huo ulitolewa wilayani humo na Mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega mara baada ya kupokea malalamiko Kutoka Kwa wananchi wake akiwa katika ziara zake za kushukuru wanakijiji hao Kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
Ulega alisema haiwezikani watu wanajimilikisha mashamba makubwa miaka hadi miaka alafu wanashindwa kuyaendelea huku wananchi wakipata shida ya kukosa maeneo hata ya kulima kilimo cha mbogamboga vijana.
"Nasema kuwa kama shamba hilo limekaa miaka yote hiyo haliendelezwi, napia huyo mwekezaji haonikani sasa mnasubiri nini kulichukua na kufanya uendelezaji,nashauri litwaeni alafu tutapambana nayo huko mbele"
Pia Ulega aliwaeleza wananchi hao kuwa siasa imekwisha na kilichobaki ni watu kufanya Kazi Kwa nguvu zote na kwamba atakuwa bega Kwa bega katika kuhakikisha maendeleo wanayapata Kwa haraka.
Awali wananchi wa kijini cha Kurutu walimweleza mbunge kuwa wanashamba kubwa ambalo alipewa mwekezaji miaka mingi iliyopita tena kienyeji lakini hadi leo ameshindwa kuliendeleza hivyo awasaidie walipate ili vijana wa eneo hilo wazalishe chumvi.
Mbunge huyo bado anaendelea na ziara zake za kutembelea kijiji hadi kijiji kwa lengo la kuwashukuru na kuhimiza shughuli za maendeleo ambapo anawataka kujituma katika kufanya kazi kwani wilaya hiyo imechelewa kimaendeleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...