Na Editha Karlo wa
Globu ya jamii,Kagera.
Globu ya jamii,Kagera.
MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa Kagera Oliver Semuguruka ametoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa waliolazwa katika hospita ya Mkoa wa Kagera.
Ametoa zawadi hizo kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi ya wanawake waliojifungua,watoto na wanawake wajawazito wanaosubiria kujifungua alisema kuwa akiwa kama kiongozi wa jamii anaguswa na masuala mbalimbali hasa yanayohusu wanawake.
"Mimi ni kiongozi wa jamii hasa wanawake,ninaguswa sana na matatizo ya wanawake wenzangu siyo wa hapa Kagera tu wanawake wa Tanzania nzima leo nimekuja kuwapa pole na nimewaletea zawadi za sabuni za kufulia,kuogea,juisi na biscuti "alisema Mbunge huyo
Akizungumzia zawadi hizo Ofisa muuguzi msaidizi wa zamu wa wodi ya wazazi Evelyne Lugabandana alimshukuru Mbunge huyo kwa msaada alitoa kwa wagonjwa.
"Tunamshukuru mbunge wetu kwa moyo wake wa upendo wa kuwakumbuka wanawake wenzake na watoto na kuamua kuja kuwapa pole na kuwapatia zawadi pia"alisema Muuguzi huyo
Baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamelazwa kwenye wodi hizo ambazo Mbunge ametoa zawadi walimshukuru mbunge kwa zawadi na kumtaka awasaidie kutatua kero waliyonayo ya kulala wawili kitanda kimoja na kwenda na vifaa vya kujifungulia.
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Kagera Oliver Semuguruka akisikiliza maelezo kutoka kwa ofisa muuguzi wa wodi ya wazazi Mkoa wa kagera kabla hajatoa zawadi kwa wodi hiyo.
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Kagera Oliver Semuguruka akiwa amembeba mmoja wa watoto aliyezaliwa kwenye hospital ta Mkoa wa Kagera alipoenda kuwasalimia na kuwapatia zawadi.
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Kagera akiwa na wajumbe wa umoja wa UWT Mkoa wa Kagera wakiwa nje ya wodi ya wazazi kabla ya kwenda kutoa zawadi kwao
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...