Msanii wa nyimbo za asili nchini Mfalme Costa Siboka ameendelea katika mikoa ya kanda ya ziwa baada ya kufanya show za nguvu kwa mashabiki wake sambamba na na promosheni ya Vuna Zawadi na Balimi extra lager.
Jumamosi hii ya tarehe 27/08 wakazi wa Nzega na vitongoji vyake kwa mara ya kwanza watampokea mfalme na nyimbo zake mpya za kinyamwezi na Kisukuma hii itakuwa mara ya kwanza kundondosha show katika mji wa Nzega.
Pia mashabiki watakaofika kwenye show zake katika miji ya Nzega, Kahama na Bariadi watapata fursa ya kuondoka na zawadi ya fulana, baisikeli na maguta.
Mfalme Siboka amewaomba mashabiki wake wajitokeze kwa wingi kwani atapiga nyimbo za makabila mbalimbali na zingine kibao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...