Na Zainab Nyamka, lobu ya Jamii.
 SHAMBULIAJI Mkongwe na nahodha wa timu ya Simba, Mussa Hassan Mgosi (Pichani)ametangaza rasmi kuachana na kusakata kabumbu na sasa anahamia upande wa benchi la ufundi, Mkongwe huyo amewahi tkucheza timu mbalimbali za ligi kuu kwa kujituma na kufikia malengo yake katika soka.

Mkuu wa kitengo cha  Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba SC, Hajji Manara amethibitisha hilo na kusema Mgosi ataagwa rasmi katika mchezo wa kirafiki kwa kimataifa utakaopigwa Jumapili ya Juma hili uwanja wa Taifa Dar es salaam dhidi ya URA ya Uganda.

Manara amesema kuwa kwa sasa Mgosi atakuwa meneja wa timu na  aliyekuwa Meneja wa timu, Abbas Suleiman Ally anakuwa Mratibu wa timu (Team Coordinator) huku kitambaa cha unahodha akikabidhiwa Jonas Gerald Mkude.

Aidha kiungo wa klabu hiyo, Peter Mwalyanzi aliyesajiliwa msimu uliopita akitokea timu ya Mbeya City FC, ametolewa kwa mkopo African Lyoni liyopanda kucheza ligi Kuu msimu huu wa 2015/2016.

Inaelezwa mechi ya Simba na  URA itakuwa ya mwisho ambapo Agosti 20 wekundu hao watashuka dimbani kukipiga na Ndanda  wakuchelechele katika uwanja wa Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...