Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama ameitaka Mifuko ya Hifadhi za jamii kuwekeza kwenye viwanda ili kuchochea uchumi wa viwanda utakaolisaidia taifa kukua kiuchumi na pia kuwanufaisha wanachama wa mifuko hiyo kutokana na uwekezaji huo wenye tija.

Jenista Amesema hayo akizungumza na Wakurugenzi wa Mifuko pamoja na Watendaji katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (ISSA) .

Amewataka Wakurugenzi hao kuunga mkono Agenda ya taifa ya kulifikisha taifa kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda.

Waziri huyo amewataka Wakurugenzi wa mifuko kuhakikisha kuwa wanadhibiti mifuko hiyo ili wanachama waweze kupata mafao yao kwa wakati muafaka bila kuwepo kwa ucheleweshaji.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (ISSA) Eliud Sanga amesema kuwa Shirikisho hilo litaendelea kuhimiza Mifuko hiyo kutimiza wajibu wake katika kutoa mafao bora kwa wanachama wao pamoja na kubuni mafao mapya ili kuwavutia wanachama.

Sanga amesema kuwa kwa sasa mifuko hiyo imefungua milango yake wazi kuwapokea wanachama kutoka sekta ambazo si rasmi ili nao waweze kunufaika na mafao . Na Pamela Mollel,Arusha.
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama akizungumza na Wakurugenzi na Watendaji wa Mifuko ya Hifadhi za Jamii katika mafunzo yaliyohusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko hiyo yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA),  jana jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (TSSA), Eliud Sanga akifafanunua jambo katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi za jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifukohhiyo.
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama akikabidhi cheti kwa Mjumbe wa Bodi ya PPF kutoka TUCTA, Adelgunda Michel aliyeshiriki katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi za jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA), jana jijini Arusha.

Katibu wa Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi za Jamii nchini (TSSA), Meshach Bandawe akizungumza katika mafunzo kwa bodi za Udhamini za Mifuko ya hifadhi za Jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko hiyo,  yaliyoandaliwa na Shirikisho hilo, jana jijini Arusha. 

Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio akisikiliza jambo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyorara.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...