Mkurugenzi
wa Jiji la Arusha Ndg. Athumani J. Kihamia amempuzisha kutekeleza majukumu yake
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji Bi.
Mwantumu Dosi kwa tuhuma za kushindwa kutekeleza majukumu yake hivyo
kukiuka kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003.
Mkurugenzi
Kihamia ametoa taarifa hiyo leo tarehe 27.08.2016 baada ya kukamilisha mbio za
Mwenge wa Uhuru na kufanya tathmini ya miradi iliyopitiwa na Mwenge na
kugundulika kwa dosari zilizojitokeza katika moja ya mradi ambao uko chini ya
Idara hii.
Mradi huo ni
kikundi cha vijana wanaojishughulisha na Uselemara pamoja na Uchomeleaji
kinachojulikana kama Mbeshere Umoja Group kilichopo Kata ya Olorieni
kiligundulika kuwa na wananchama waliovuka umri wa miaka 35 ambao hawastahili
kunufaika na Mikopo ya Vijana kwa mujibu
wa Sera.
Mwenge wa
Uhuru katika Jiji la Arusha ulikimbizwa tarehe 24.08.2016 na Kikundi hicho
kilikua ni miongoni mwa miradi iliyokua inapitiwa na Mwenge wa Uhuru ambapo
wanachama wake hawakizi vigezo. Wanachama hao walikua wameandaliwa kupewa Hundi
ya TSH Milioni tano kama ishara ya kuunga mkono jitihada zao zakuboresha
maisha. Mkimbiza Mbio za Mwenge Kitaifa
Ndg. George Jackson Mbijima alisitisha zoezi hilo baada ya kugundua dosari za
umri kwa baadhi ya wanachama.
Kupumzishwa
kutekeleza majukumu ya Mkuu wa Idara hii kunafuatana na masharti ya kukabidhi
Ofisi kwa Mratibu wa Tasaf Bi. Tajiel
Mahega ambaye kwa sasa atakua Kaimu Mkuu
wa Idara hii mpaka pale uchunguzi
utakapokamilika.
Nteghenjwa Hosseah
Afisa Habari, Halmashauri ya Jiji
Arusha.
27
Agosti,2016
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...