Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Mh. Paul William Mtima Akikata utepe katika Uzinduzi Wa kampuni ya Mobisol kwa nyanda za juu kusini hivi katibuni iliyopo Soweto Block "C" Jijini Mbeya.

 

 Mobisol ni kampuni yenye asili ya Ujerumani inayoongoza kwa kutengeneza, kusambaza na kuuza Mitambo ya Umeme wa Jua (Sola) iliyo salama kiafya na mazingira katika ubora wa hali ya juu, Ikiwa mbadala wa nishati isiyo salama  kwa gharama nafuu kwa watu wa vipato vyote.

Mchezaji wa timu ya Ilemi Fc, Rajabu Jezi ya bluu bahari akijaribu kuwatoka wachezaji wa timu ya Msumari wa Moto katika mchezo ulio chezwa hivi karibuni katika viwanja vya shule ya msingi mwenge na kutoka sare ya bila kufungana  ikiwa ni muendelezo wa ligi ya Mobisol inayo endelea hivi sasa mkoani mbeya kwa udhamini mkubwa wa Mobisol Mabingwa wa nishati ya umeme wa Jua "Sola" Tanzania.

Kwakutambua na kupenda kuendelea kuenzi mahusiano mazuri na Wakazi wa Nyanda za juu kusini, Mobisol  Mobisol ambao ndio wadhamini wakuu wa Ligi ya Mobisol Cup iliyoshika Kasi jijini Mbeya Ikihusisha Timu 20 Kutoka Mbeya Jiji, Mbeya Vijijini  na Wilaya ya Chunya, Tarehe 13/08/2016  Ilifanya ufunguzi rasmi wa kuanza kufanya kazi Kanda ya nyanda za juu kusini uliofanyika Katika ofisi zao za kanda zilizopo Soweto Block C mkabala na jengo la Oilcom.

Mtanange Ukiendelea kwa udhamini mkuu wa Mobisol

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...