Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo

Na Woinde Shizza, Arusha
 Mchimbaji wa kisima aliyefahamika kwa majina ya Waziri Omary (25) mkazi wa Ngaramtoni amefariki dunia kisimani wakati akichimba kisimani.
Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amekiri kutokea kwa tukio hilo marehemu alikutwa amefariki kisimani baada ya  kuwasha moto wa mkaa ili kulainisha mwamba ili aweze kupata maji kwenye kisima  chenye urefu wa futi 60, alikutwa saa 5 juzi akiwa ameshapoteza maisha.
"Kilichotokea ni kwamba huenda wakati amewasha jiko, Carbonmonoxide ilizidi huku hewa ya Oxygen ilikuwa ndogo kiafya lazima angedhurika. Mwili wa marehemu haujakutwa na jeraha  lolote, tunaendelea na uchunguzi kubaini zaidi , "alisema Kamanda. Pia amewatahadharisha watu kuhakikisha watu nawapotumia majiko ya mkaa ndani kuhakikisha kuna hewa ya kutosha..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...