Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

Dar es salaam

Tofauti za kisiasa zilizopo nchini zisivuruge nuru ya amani iliyojengwa tangu enzi za Serikali ya Awamu ya Kwanza ambapo siasa za nchi zililenga katika umoja, amani na ujenzi wa Taifa imara, anaonyesha mmoja wa walimu wa diplomasia nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia nchini (CFR), Dkt. Bernard Achiula wakati wa mahojiano na Mwandishi wa habari hii kuhusu hali ya siasa nchini kwa sasa na ushiriki wa watanzania kwa ujumla katika kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano katika utatuzi wa changamoto za kimaendeleo badala ya kuanzisha tabia za vurugu na maandamano.

Dkt. Achiula amesema kuwa uwepo wa amani nchini unachangia katika kuvutia wawekezaji  nchini, kukuza utalii wa ndani, kuvutia wahisani kutoa misaada kwa kuchangia katika uanzishaji na uendelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo kila raia nchini bila kujali itikadi yake ya dini wala chama ana budi kuilinda amani iliyopo.

“Tofauti za kisiasa zipo katika kila nchi kulingana na mitazamo tofauti iliyopo ila kinachotakiwa ni kuweka taifa mbele kwa manufaa ya nchi, watanzania tunatakiwa kuwa wazalendo ili kuimarisha umoja na amani iliyopo kwani vitu hivi vinategemeana na hatimaye kuiwezesha Serikali ya awamu ya tano kuwatumikia wananchi kwa kuwaletea maendeleo.

“Tofauti hizo zisiwe chachu ya kuvuruga amani tuliyonayo bali watanzania kwa ujumla tunatakiwa kuitunza amani hii iliyojengwa tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere ili kuweza kuvutia wawekezaji na  utalii katika nchi yetu” alifafanua Dkt Achiula.

Alisema kuwa haoni sababu kwa vyama vya siasa nchini kuandaa maandamano yanayolenga kuvuruga amani iliyopo kwani kikubwa kinachotakiwa kwa wananchi ni misingi mikuu ya maendeleo ikiwemo elimu, afya na huduma bora mbalimbali  ambapo Rais Magufuli ameanza kuvifanyiakazi. 

Akizungumza kuhusu Balozi zetu nje ya nchi Dkt Achiula aliwashauri mabalozi hao kuzidi kuitanganza nchi yetu ya Tanzania ili kuweza kuvutia wawekezaji, utalii na biashara ili kusaidia katika ukuuaji wa sekta ya viwanda ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuipeleka nchi katika uchumi wa viwanda.

Akizungumzia utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano Dkt Achiula amesema kuwa Rais Dkt. Magufuli amejikita katika kutatua changamoto zinazolikabili taifa kwa muda mrefu ikiwemo kupiga vita rushwa, kuongeza ukusanyaji mapato kwa kuwabana wakwepa kodi, kubana matumizi ikiwa nia ni kuimarisha uchumi wa nchi na kuipeleka nchi kwenye uchumi wa Kati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa


  1. Naunga mkono kwamba hakuna sababu ya maandamano hasa pale yanapokuwa yamepigwa marufuku na utawala. Jambo la msingi ni kusulisha migororo kwa mazungumzo na vyombo kama mabaraza mbali mbali likiwepo Bunge.

    Nadhani ni haki "KUBWA" sana ya Kikatiba kwa Wawakilishi wetu kutumia chombo hiki kutatua matatizo ya Taifa hili kuliko haki ya Kikatiba ya kuandamana.

    Binafsi nampongeza Dkt Achiula hasa pale aliposema haijalishi ni jumuiya ngapi sisi kama nchi tumejiunga bali swali la kujiuliza ni Tunajua tunachokitaka katika hizo jumuiya?

    Nawasilisha.

    ReplyDelete
  2. kusingetolewa amri ya kuzuia mikutano na maandamano bila shaka tusingefika hapa. Mwalimu Nyerere alipata kutuasa tuwe na utaratibu wa kujisahihisha. Kinachotakiwa kuruhusu mara moja na bila masharti yoyote mikutano na maandamano na nina hakika hilo likifanyika huu mzozo na tishio la amani yetu halitakuwepo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...