Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini Profesa James Mdoe ametembelea mnada wa Madini ya Tanzanite yaliyochimbwa kutoka migodi ya Kampuni tano za wafanyabiasha wa madini hayo ili kuona utaratibu unaotumika kuwapata washindi wa zabuni za kununua madini ya hayo wakati wa mnada.

Mnada huo unatarajia kufanyika Agosti 12 mwaka huu na unafanyia Tanzania kwa mara kwanza; Vilevile watakaoshinda zabuni za kununua madini ya hayo watatangazwa wakati wa mnada.Mnada huo umeshirikisha wafanyabiashara wa Madini wa ndani na nje ya Tanzania.

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Madini wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe ( kushoto) akionyeshwa namna ya kutambua ubora wa jiwe la Tanzanite na Mkurugenzi wa Uthaminishaji na Almasi na vito Tanzania( TANSORT) Archard Kalugendo( kulia).

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Madini wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe akitazama ubora wa jiwe la Tanzanite kupitia kifaa maalim.
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Madini wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe( kushoto )akizungumza na baadhi ya wauzaji wa Madini ya Tanzanite, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya VGL Group ,Sunil Agrawal( kulia), na Mmoja wa Wakurugezi wa Kampuni ya TanzaniaOne, Rizwan Ullah ( wa pili kulia) wakati wa mnada wa Madini ya Tanzanite mkoani Arusha.
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Madini wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe ( kushoto)akielezwa utaratibu wa kujaza fomu za kushiriki Mnada wa madini ya Tanzanite utakaofanyika Agosti 12 mkoani Arusha,kutoka kwa Mhandisi Juma Lunda( katikati) na Sekretari wa kituo cha Jimolojia Tanzania ( TGC)Halima Hussein(kulia) mnada huyo utafanyika Tanzania kwa mara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...