Mmoja kati ya Wakurugenzi wa Peacock Hotel,Daniel Mfugale akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya uzinduazi wa mtanao wa kijaamii unaolenga kutangaza chakula cha asili cha Mtanzania leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wafanyakazi wa hotel hiyo waliofika kwenye uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).

Uongozi wa Peacock Hotel umezindua rasmi mtandao wake wa kijaamii unaolenga kutangaza chakula cha asili cha Mtanzania.

Mmoja kati ya Wakurugenzi wa Hotel hiyo Daniel Mfugale alisema kuwa uamuzi huo umefanyika baada ya kuona mitandao ya kijamii sasa inasambaza taarifa haraka na kuwafikia watu wengi nje na nchi hivyo itasaidia kuongeza utalii Nchini.

“Kwa sasa mitandao ya kijamii ndiyo imeshika hatamu kwa usambazaji wa taarifa hivyo huduma yetu iitwayo Usiku wa Mtanzania ambayo ni maalumu kwa chakula cha asili cha makabila yote nchini itakua inatangazwa katika kurasa zetu za facebook na Instagram tulizozifungua leo”, alisema Mfugale. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...