Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akizungumza na wanachama wa Kataa Unene Family (KUF) jumapili Agosti 7, 2016 wakati wa maadhimisho ya miaka 3 tokea umoja huo kuanzishwa. Pembeni kulia ni Kiongozi wa Kataa Unene Family Bi. Angela Msangi na Bi. Mariam Sagini Bi. Mariam Sagini (kushoto) Mshindi wa shindano la kupunguza kilo 10 kwa muda wa miezi mitatu.





Kundi la Kataa unene (KUF) linalojihusisha na kupunguza unene kwa mazoezi na kula vyakula bora limeadhimisha miaka 3 kwa na kuweka mikakati mipya ya kuwasaidia wengine.
Akizungumza katika sherehe hiyo iliyofanyika Epidor Masaki, jijini Dar es Salaam, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda ambaye alipita kuwasalimia alilipongeza kundi hilo huku akisema kuwa afya ni msingi wa maendeleo yoyote duniani, hivyo hatua ya kutambua kujiweka imara mapema ni njema.
"Nawapongeza sana kwa moyo mlionao wa kufanya mazoezi si jambo dogo maana linahitaji nidhamu ya hali ya juu ... kujisimamia mwenyewe bila kushinikizwa na mtu,' alisema Mhe. Makonda.
Kiongozi wa Kataa Unene Family Bi Angela Msangi (katikati) akiwakaribisha wanachama wenzake wa Kataa Unene Family wakati wa maadhimisho ya miaka mitatu ya KUF yaliyofanyika Jumapili Agosti 7, 2016 jijini Dar es Salaam. Pembeni kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Nidhani ya KUF, Bi. Etty Kusiluka na Bi. Mariam Sagini (kushoto) Mshindi wa shindano la kupunguza kilo 10 kwa muda wa miezi mitatu.
Aidha, alieleza kuwa viwanja vya michezo jijini Dar es Salaam vipo vingi, maeneo ya wazi pia hivyo kuwasihi wananchi kujihusisha katika mazoezi, huo wao kama viongozi wakiwaunganisha na makundi mengine ya michezo kwa mashindano kama Toto cup, Ndondo cup na mengineyo, hasa wanafunzi wa vyuoni na shule za msingi.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Kataa Unene Family Bi Angela Msangi alisema katika miaka mitatu, tayari watu zaidi ya 40 wamepunguza kuanzia kilo 15 hadi 25, ambapo tayari watu 10 wamefikia malengo ya kilo zinazohitajika kutokana na urefu wao na wanaendelea kujidhibiti.
  Wanachama wa KUF wakimpongeza Mjumbe wa Kamati ya Nidhani ya KUF, Bi. Etty Kusiluka wakati akiwapa ujumbe.

Angela alisisitiza kuwa, kupungua kwa kufanya mazoezi na kula vyakula vinavyofaa na kushauriwa kunawezekana endapo tu mtu ataamua kujikana na kudhamiria,akiwaondoa watu fikra potofu kuwa wanaopungua wanatumia dawa.
Shughuli hiyo ya Kataa Unene ilienda sambamba na kutoa zawadi kwa waliofanya vizuri katika shindano la kupungua la miezi mitatu iliyopita, lililopewa jina la Sagini challange,ambapo aliyeibuka kinara wa shindano hilo ni muasisi wa shindano Mariam Sagini, aliyepunguza kilo 10 tangu mwezi Mei mwaka huu.
Bi. Mariam akiwaonyesha wenzake jinsi gauni lake lilivyomkaa vyema baada ya kupungua kilo 10 kwa muda wa miezi mitatu.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. hiki chama ni kizuri kwa kuwaelimisha wananchi na pia kudumisha afya.
    Nawashauri pia wasitumia uzito (kg) kwa kupima afya bali pia BMI (uwiani wa uzito na urefu).

    Hasa, BMI.

    ReplyDelete
  2. Website yao iko wapi niwatanganze?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...