Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akizungumza na wanachama wa
Kataa Unene Family (KUF) jumapili Agosti 7, 2016 wakati wa maadhimisho
ya miaka 3 tokea umoja huo kuanzishwa. Pembeni kulia ni Kiongozi wa
Kataa Unene Family Bi. Angela Msangi na Bi. Mariam Sagini Bi. Mariam
Sagini (kushoto) Mshindi wa shindano la kupunguza kilo 10 kwa muda wa
miezi mitatu.
Kundi la Kataa unene (KUF) linalojihusisha na kupunguza unene kwa mazoezi na kula vyakula bora limeadhimisha miaka 3 kwa na kuweka mikakati mipya ya kuwasaidia wengine.
Kundi la Kataa unene (KUF) linalojihusisha na kupunguza unene kwa mazoezi na kula vyakula bora limeadhimisha miaka 3 kwa na kuweka mikakati mipya ya kuwasaidia wengine.
Akizungumza
katika sherehe hiyo iliyofanyika Epidor Masaki, jijini Dar es Salaam,
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda ambaye alipita
kuwasalimia alilipongeza kundi hilo huku akisema kuwa afya ni msingi wa
maendeleo yoyote duniani, hivyo hatua ya kutambua kujiweka imara mapema
ni njema.
"Nawapongeza
sana kwa moyo mlionao wa kufanya mazoezi si jambo dogo maana linahitaji
nidhamu ya hali ya juu ... kujisimamia mwenyewe bila kushinikizwa na
mtu,' alisema Mhe. Makonda.
Kiongozi
wa Kataa Unene Family Bi Angela Msangi (katikati) akiwakaribisha
wanachama wenzake wa Kataa Unene Family wakati wa maadhimisho ya miaka
mitatu ya KUF yaliyofanyika Jumapili Agosti 7, 2016 jijini Dar es
Salaam. Pembeni kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Nidhani ya KUF, Bi. Etty
Kusiluka na Bi. Mariam Sagini (kushoto) Mshindi wa shindano la kupunguza
kilo 10 kwa muda wa miezi mitatu.
Aidha,
alieleza kuwa viwanja vya michezo jijini Dar es Salaam vipo vingi,
maeneo ya wazi pia hivyo kuwasihi wananchi kujihusisha katika mazoezi,
huo wao kama viongozi wakiwaunganisha na makundi mengine ya michezo kwa
mashindano kama Toto cup, Ndondo cup na mengineyo, hasa wanafunzi wa
vyuoni na shule za msingi.
Kwa
upande wake, Kiongozi wa Kataa Unene Family Bi Angela Msangi alisema
katika miaka mitatu, tayari watu zaidi ya 40 wamepunguza kuanzia kilo 15
hadi 25, ambapo tayari watu 10 wamefikia malengo ya kilo zinazohitajika
kutokana na urefu wao na wanaendelea kujidhibiti.
Wanachama wa KUF wakimpongeza Mjumbe wa Kamati ya Nidhani ya KUF, Bi. Etty Kusiluka wakati akiwapa ujumbe.
Wanachama wa KUF wakimpongeza Mjumbe wa Kamati ya Nidhani ya KUF, Bi. Etty Kusiluka wakati akiwapa ujumbe.
Angela
alisisitiza kuwa, kupungua kwa kufanya mazoezi na kula vyakula
vinavyofaa na kushauriwa kunawezekana endapo tu mtu ataamua kujikana na
kudhamiria,akiwaondoa watu fikra potofu kuwa wanaopungua wanatumia dawa.
Shughuli
hiyo ya Kataa Unene ilienda sambamba na kutoa zawadi kwa waliofanya
vizuri katika shindano la kupungua la miezi mitatu iliyopita, lililopewa
jina la Sagini challange,ambapo aliyeibuka kinara wa shindano hilo ni
muasisi wa shindano Mariam Sagini, aliyepunguza kilo 10 tangu mwezi Mei
mwaka huu.
Bi. Mariam akiwaonyesha wenzake jinsi gauni lake lilivyomkaa vyema baada ya kupungua kilo 10 kwa muda wa miezi mitatu.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
hiki chama ni kizuri kwa kuwaelimisha wananchi na pia kudumisha afya.
ReplyDeleteNawashauri pia wasitumia uzito (kg) kwa kupima afya bali pia BMI (uwiani wa uzito na urefu).
Hasa, BMI.
Website yao iko wapi niwatanganze?
ReplyDelete