Na Bakari Issa Madjeshi, Globu ya Jamii
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amekabidhi mchoro wa ramani
wenye ghorofa tatu kwa uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu nchini,BAKWATA
ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza hilo.
Pamoja
na kukabidhi ramani hiyo, Mkuu wa Mkoa huyo amesema jengo hilo
litagharimu kiasi cha fedha 5, 080, 155, 600 ili kukamilika. Pia amesema
jengo hilo mpaka kukamilika litakuwa la kipee na kupewa hadhi kama
Taasisi kubwa ya Kiislamu na kusisitiza ujenzi wa jengo hilo hautazidi
miezi 14.
Amesema amekabidhi mchoro huo kutokana na kutambua na kuthamini umuhimu wa BAKWATA katika Taifa pamoja na kuwataka Waislamu na wasiokuwa waislamu kujitokeza katika kutoa misaada hiyo. Pia ametoa shukrani kwa waislamu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa kushereheka nao pamoja katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambapo amesema mwezi huo ndio uliokuwa chimbumbo la ujenzi wa jengo hilo la BAKWATA.
Amesema amekabidhi mchoro huo kutokana na kutambua na kuthamini umuhimu wa BAKWATA katika Taifa pamoja na kuwataka Waislamu na wasiokuwa waislamu kujitokeza katika kutoa misaada hiyo. Pia ametoa shukrani kwa waislamu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa kushereheka nao pamoja katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambapo amesema mwezi huo ndio uliokuwa chimbumbo la ujenzi wa jengo hilo la BAKWATA.
Akitoa
shukrani zake kwa Mkuu wa Mkoa huyo, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti
Abuubakari Zuberi amewataka Waislamu kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa huyo
ikiwa kuwataka kuamini ya kuwa na haki ya kupokea misaada kama Waislamu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akimuelekeza jambo Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti,Abubakary Zubeir namna ujenzi wa ghorofa hilo utakavyokuwa,mara baada ya kukabidhiwa mchoro wa jengo hilo litakalogharimu zaidi bilioni tano,kulia ni Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam , Alhaji Mussa Salum.PICHA NA MICHUZI JR.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pampja na Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti,Abubakary Zubeir wakitazama mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu,ambapo ujenzi wake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni tano,ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza hilo.
,kulia ni Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam , Alhaji Mussa Salum .
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pamoja naSheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti wakionesha mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu kwa wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo fupi iliyofanyika jijini Dar mapema leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizaungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu kwa uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu nchini,BAKWATA ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza hilo.
Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti Abubakary Zubeir akifafanua jambo mbele ya wageni waalikwa,kabla ya kukabidhiwa mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu kwa uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu nchini,BAKWATA ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya la Baraza hilo.
Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam , Alhaji Mussa Salum akimkaribisha Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti Abubakary Zubeir mbele ya wageni waalikwa,kabla ya kukabidhiwa mchoro wa ramani wenye ghorofa tatu kwa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar ES Salaam,Mh Paul Makonda.
Baadhi ya Wageni waalikwa wakifuatilia yalikuwa yakijiri kwenye hafla hiyo fupi.
Baadhi ya Wageni waalikwa wakifuatilia yalikuwa yakijiri kwenye hafla hiyo fupi.
Napenda kuuliza tukianza kutumia pesa za umma kwa mambo kama haya je tupo tayari kuwajengea taasisi zote nyinginezo za dini??? Na hii bilioni 5 inatokea wapi??
ReplyDeleteHuu ni mtazamo mwema tu kwa manufaa ya Taifa langu nalolipenda la Tanzania na sina niha mbaya na kama nimekosea ningeomba kuelimishwa. Ila kama zinatokea Serikalini (iwe kuu au ya mkoa) ipo wapi dhana ya Serikali kutokuwa na dini? Na ukianza jambo basi tujiandae kufanya mengineyo...