Bia ya kopo ya kwanza yenye ujazo wa mililita 500 kwa bia ya Kitanzania.
Kampuni
ya Bia ya TBL kupitia bia yake ya Safari lager imezindua bia ya kopo ya kwanza yenye
ujazo wa mililita 500 kwa bia ya Kitanzania. Akizungumza katika uzinduzi
uliofanyika jijini Dar, Meneja Bidhaa wa Safari Lager, Edith Bebwa Nasuwa
alisema “Ni bia ya kwanza ya Kitanzania ya kopo yenye ujazo wa mililita 500
ambayo italeta urahisi, unafuu na ladha nzuri ya aina yake kwa wapenzi wote wa
bia ya Safari Lager” Bia hii ya kopo tayari imeshaanza kupatikana maeneo yote nchini kuanzia tarehe 26 Agosti 2016 na imeelezewa kuwa ni bia ya wajanja wenye kujiamini.
“Bia mpya ya kopo ya Safari ni dhahiri kwamba imetengezwa kumpa umahiri Mtanzania katika safari ya maisha yake. Inapatikana kwa urahisi na kwa wakati muafaka hata wakati mtu anakwenda kwenye mihangaiko yake au kubeba akiwa anakwenda kwenye matembezi au safarini” alimalizia Edith Bebwa.
Fuatilia kurasa za Safari Lager kupata habari zaidi
Facebook: https://web.facebook.com/SafariLagerTz
Bia ya kopo ya kwanza yenye ujazo wa mililita 500 kwa bia ya Kitanzania.
Wadau wakifurahia bia ya kopo ya kwanza yenye ujazo wa mililita 500 kwa bia ya Kitanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...