Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dk. Bakari Jabiri akitoa ufafanuzi kwa Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (kulia) kuhusu kituo cha ufuatiliaji mifumo ya mawasiliano Serikalini, Ofisi za Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA) jijini Dar es salaam.

Na Aron Msigwa – MAELEZO.

Matumizi ya Teknolojia ya Habari na mawasiliano (TEHAMA) katika uendeshaji wa shughuli za serikali ( e-Government) katika miaka ya hivi karibuni yameendelea kukua kwa kasi na kupata nguvu katika nchi mbalimbali duniani kutokana na mchango wake katika kufanikisha utoaji wa taarifa na huduma kwa wananchi kwa haraka na gharama nafuu.

TEHAMA imegusa maisha ya kila siku ya wananchi na kurahisisha mawasiliano muhimu katika shughuli zao kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa na kijamii. Aidha, TEHAMA imekuwa mkombozi katika kurahisisha na kuimarisha sekta ya biashara na fedha.

Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2014 kuhusu matumizi ya Mtandao katika shughuli za Serikali ( 2014 UN e- Government Survey) kwa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa inaonesha kuwa matumizi ya TEHAMA kwenye shughuli za Serikali duniani kote yamefanikiwa sana kuwasogeza wananchi karibu na Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...