Mwenyekiti wa Bodi wa Shule za Feza, Habib Miradj akizungumza na waandishi wa habari juu kuhusiana na taarifa zinazozagaa za kufungwa kwa shule za Feza leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkuu wa shule wa Feza, kadri dalcicea.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SHULE za Feza nchini hazitafungwa kutokana na shule hizo zimesajiliwa kwa mujibu wa sheria za nchi hivyo ikibidi kufanya hivyo sheria zitatumika zilezizle zilizofanya shule hizo zisajiliwe.

Hayo ameyasema leo Mwenyekiti wa Bodi wa Shule za Feza, Habib Miradj wakati alipokutana na waandishi wa habari leo juu ya kuzagaa kwa taarifa katika mitandao si michuzi blog juu ya shule za fedha kufungwa, amesema kuwa taarifa hizo hazina ukweli na kuwataka wazazi kuendelea kuwaunga mkono katika kusukuma gurudumu la elimu.

Amesema Feza imekuwa ikijulikana kimataifa kwa kufanya vizuri na kuweza kupata tuzo mbalimbali katika utoaji wa elimu ikiwa na wanafunzi wanaokwenda katika vyuo vya ndani ya nje wamekuwa wakipata ufaulu wa juu.

Miradj amesema kuwa wakaguzi shule wamekuwa wakienda na kuwashauri vitu mbalimbali hivyo hata kufungwa kwa sheria zitatumika lakini  suala hilo halitegemei kutokea  katika shule zetu za feza kutokana na hadhi ambayo imefikia katika utoaji wa elimu.

Aidha amesema kuwa Feza inazidi kujiimarisha katika utoaji wa elimu na kuongeza kuwa mpango wao kuhakikisha shule zinaongezeka katika baadhi ya maeneo kutokana na mahitaji ya elimu nchini.

Amesema historia ya Feza imetokana na juhudi za serikali ya kutaka uwekezaji  wa shule ufanywe nchini baada kuonekana kufanya vizuri nchini Uturuki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...