Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba akizungumza Katika uzinduzi wa ripoti yahali ya afrika mashariki 2016 kukosekana kwa usawa katika masuala ya kuiuchumi na kisiasa (The state of East Africa 2016 consolidating Misery, the political economy of inequalities) jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Society International Development (SID), Ali Hersi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Katika uzinduzi wa ripoti yahali ya afrika mashariki 2016 kukosekana kwa usawa katika masuala ya kuiuchumi na kisiasa jijini Dar es Salaam leo.
Kutoka kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba,  Mkurugenzi Msaidizi wa Society International Development (SID), Ali Hersi, Mkurugenzi Msaidizi wa Society International Development (SID), Arthur Muliro na Meneja Mradi (TMEA), Monica Hangi wakionesha Ripoti ya hali ya afrika mashariki 2016 ya  kukosekana kwa usawa katika masuala ya kuiuchumi na kisiasa.
Katika hafla ya uzinduzi wa Ripoti Hiyo jijini Dar es Salaam leo.

KATIKA kuhakikisha jamii ya Tanzania inakuwa na usawa katika ukuwaji wauchumi, jamii imeshauriwa kuwekeza katika elimu ilikuweza kuondokana na pengo la walionacho nawasiokuwanacho ili kukuza uchumi na kukuza kipato chao .
.
Akizungumza Katika uzinduzi wa ripoti yahali ya afrika mashariki 2016 kukosekana kwa usawa katika masuala ya kuiuchumi nakisiasa (The state of East Africa 2016 consolidating Misery, the political economy of inequalities) Waziri wa Mazingira ofisi ya makamu wa Rais January Makamba amesema kuwa hali ya umasikini imezidi kuwa kubwa hali inayochangiwa na hali ya kuwepo kwa pengo walionacho nawasikiuwa nacho kuwa kubwa .

‘Changamoto kubwa tangu tupate uhuru ni umasikini,ujinga maradhi  lakini ameongezeka adui mwingine kati ya walionacho na wasikuwa nacho lakini kutkana nauzinduzi wa ripoti hii itakuwa mwarobaini wa hali ya pengo la walionacho nawasikuwa nacho’Alisema Waziri wa Mazingira ofisi ya Makamu wa Rais January Makamba.

Waziri Makamba amesema kuwa hali ya kuwepo kwa pengo la walionacho nawasikuwa nacho kuongezeka limetokana na kukosekana kwa usawa wa ugawaji wa rasmali hali hiyo inapotekea nilazima viongozi wawemakini katika kudhibiti hali hiyo .

Amesema kuwa Hapo awali usawa wakipato ulikuwa unachangiwa nadhana malimbali ikiwemo Rangi ambapo jamii ya kiasia nawazungu walikuwa wakimiliki kiwango kikubwa cha Rasmali ikilinganishwa na waafrika ambao walikuwa wakimiliki kiwango kidogo cha Rasmali .

‘’KATIKA safari yanchi yetu tumepata wazungu wapya,kuna watumishi wanaishi maisha mazuri tofauti ya kipatohatuna budi kukabiliana natatizo la usawa kwa kuwekeza kwenye elimu kwani ninyenzo muhimu lakukabiliana natatizo lakukosekana kwa usawa’Amesema Makamba.

Makamba ameongeza kuwa takwimu zinaonesha kuwa uchumi watanzania unakuwa siku hadi siku nilazima kuwekeza kwa elimu kwa watoto wetu ilikuondokana napengo lawalionacho nawasikuwa nacho hali itakayo chochea ukuwaji wa kiuchumi na kuondokana umasikini wakipato .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...