Mwananchi aliyefika katika banda la Huduma ya Afya ya Macho akifanyiwa uchunguzi wa Macho katika maadhimisho ya sherehe za Nane Nane mkoani Lindi leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mheshimiwa George B. Simbachawene alipotembelea banda la Sightsavers na idara ya afya mkoa akisikiliza kwa makini maelezo ya shughuli zinazofanywa na washirika hawa ili kutokomeza ugonjwa wa vikope mkoani Lindi hadi sasa jumla ya wagonjwa 830 wamekwisha pata usawaziswaji wa vikope mkoa wa Lindi. Katika wilaya ya Ruangwa na Nachingwea, kulia akizungumza Dr. Leonard Ndeki afisa mradi kutoka shirika la Sightsavers Tanzania katikati mwenye T-Sheti ya bluu ni Dr. Mwita Machage Mratibu wa Huduma za Macho Mkoa wa Lindi

Timu ya washiriki toka shirika la Sightsavers na watumishi wa Idara ya Macho Mkoa wa Lindi waliokaa wakiendelea kutoa huduma ya uchunguzi wa macho, Ushauri na Tiba kwa wananchi wa mkoa wa Lindi. Kutoka kushoto Dk. Mwita Machage, Dk. Leonard Ndeki (Sightsavers), Bw. Richard Shaban na aliyesimama mwenye T-Shirt nyeusi ni Zera Ombeni.
Baadhi ya wanawake na wanaume wa mkoa wa Lindi waliofika kwenye banda la Sightsavers na Idara ya afya mkoa kupata huduma ya macho wakisubiria kupata huduma wakisubiri kuhudumiwa na wataalam wa Macho. 


HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...