TIMU ya Simba imeweza kutoka na ushindi mnono wa magoli 4-0 dhidi ya AFC Leopards kutoka nchini Kenya, mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikiwa ni maadhimisho ya miaka 80 ya tangu kuanzishwa kwa timu ya Simba.

Simba iliweza kutawala mchezo kwa kiasi kikubwa ambapo dakika ya 38 Ibrahim Ajib aliipatia Simba bao la kuongoza baada ya kupokea pasi safi toka kwa Jonas Mkude na kuachia shuti la chini chini umbali wa kama mita 25.

Kipindi cha pili Simba iliwaingiza Muzamir Yassin, Jamal Mnyate na Laudit Mavugo ambao walibadilisha mchezo kwa kiasi kikubwa kwa kuongeza mashambulizi na kuwafanya mabeki wa Leopards kuwa 'bize' muda wote kupambana na washambuliaji wa simba jambao ambalo lilishindwa kufua dafu mbele ya washambuliaji hao.

Dakika ya 55 Ajib tena anaifungia Simba goli la pili baada ya Mavugo kuichambua vyema safu ya ulinzi ya Leopards na kumrahisishia mfungaji.

Dakika kumi baadae Kichuya alifungia Simba goli la tatu baada ya kupokea mpira wa krosi uliopigwa kiufundi na Mavugo.

Ilichukua kama dakika saba hivi baada ya goli la tatu, pale Mavugo alipoifungia timu yake goli la nne baada ya kumalizia kazi kubwa iliyofanywa na Kichuya ambaye aliwafanya mabeki wa Leopards kuwa nae macho muda wote.

Mashabiki wa Simba waliohudhuria mchezo huo wameonesha imani kubwa kwa kikosi chao hicho kilichosukwa chini ya Omog kwa ushirikiano na Jackson Mayanja.
Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Laubit Mavugo akishangilia mara baada ya kuipatia timu yake bao la Nne dhindi ya Wageni wao, AFC Leopards ya Nchini Kenya, wakati wa Mtanange wao wa kirafiki ulioambatana na sherehe za kuadhimisha Miaka 80 ya tangu kuanzishwa wa timu ya Simba a.k.a Wekundu wa Msimbazi, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Hadi kipenda cha mwisho kilipolizwa na Mwamuzi, Heri Sasi, Simba ilikuwa ishaichakaza AFC Leopards kwa Bao 4 - 0. 
Nahodha wa Timu ya Simba, Jonas Mkude akiangalia namna ya kumtoka Mchezaji wa Timu ya AFC Leopards ya nchini Kenya, Bernard Ongoma, wakati wa Mtanange wao wa kirafiki ulioambatana na sherehe za kuadhimisha Miaka 80 ya tangu kuanzishwa wa timu ya Simba a.k.a Wekundu wa Msimbazi, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam.Simba imeshinda 4-0.
Mgeni Rasmi katika Sherehe za kuadhimisha Miaka 80 ya Simba, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiongozana na viongozi mbali mbali wa Timu ya Simba kuingia uwanjani kuwasalimia Wachezaji pamoja na Washabiki waliofurika kwa wingi uwanjani hapo.
Msemaji wa Timu ya Simba, Haji Manara akitoka kuwasabahi mashabiki wa Simba waliofurika uwanja wa Taifa leo.
Wanamuziki wa Bendi ya Twanga Pepeta wakitoa Burudani uwanjani hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jamani Simba wenzangu mambo yasiishie kwenye keki,tunataka raha msimu huu Msimbazi,tuwe kitu kimoja

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...