SIMU.TV:  Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Salumu Happy ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa mganga mfawidhi wa hospitali ya Mwananyamala kwa kupandisha bei ya matibabu kinyume na utaratibu. https://youtu.be/S3ZIe2CIrTI

SIMU.TV:  Rais Dr John Pombe Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa jumuiya ya Afrika mashariki amekutana na katibu mkuu wa jumuiya hiyo balozi Liberata Mfumukeko na kujadili namna ya kukabilina na matatizo ya jumuiya hiyo.https://youtu.be/bWf6alU0mFw

SIMU.TV:  Waziri mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa wilaya na maafisa elimu nchini kufanya ukaguzi wa wanafunzi katika shule zote ili kubaini udanganyifu wa idadi ya wanafunzi. https://youtu.be/9EVcmk2RaV0

SIMU.TV:  Wakazi wa mji mdogo wa Hydom wilayani Mbulu wamekua wakitaabika na upataikanaji wa huduma ya maji huku mkandarasi wa mradi wa maji akitokomea kusikojulikana. https://youtu.be/X6Qrb_yA94Y

SIMU.TV:  Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani likishirikiana na kampuni ya Makini Application wamezindua huduma ya kumuwezesha abiria kujua mwendo wa gari alilopanda kwa kutumia simu yake ya mkononi. https://youtu.be/hHr3rZsTyzI

SIMU.TV:  Chama cha wamiliki wa mabasi nchini TABOA kimesema kitasitisha huduma ya usafiri kuanzia agosti 22 kwa ajili ya kupisha zoezi la ukaguzi wa mabasi.https://youtu.be/dL1-laXQa_o

SIMU.TV:   Wafugaji wa jamii ya Kimang’ati wanaoishi katika wilaya ya Bagamoyo wameiomba serikali kukaa nao na wakulima ili kumaliza migogoro yao na wakulima.https://youtu.be/zD_WUjdiTtw

SIMU.TV:  Wafanyabiashara na wavunaji wa misitu nchini wametakiwa kufanya kazi hiyo kwa utaratibu wenye tija kwa taifa na kwa vizazi vijavyo. https://youtu.be/FmHbflWIgH8

SIMU.TV:  Wafanyabiashara wadogo wa mazao wameiomba serikali kusimamia bei za mazao kutokana na baadhi ya mazao kutokua na bei yenye msimamo.https://youtu.be/jfFsUvV76-4

SIMU.TV:  Mfuko wa hifadhi ya jamii wa LAPF imeeleza nia yake ya kuwekeza katika viwanda vidogo vyenye tija baada ya kufanya upembuzi yakinifu.https://youtu.be/TcbGX_0Hzts

SIMU.TV:  Klabu ya soka ya Ndada fc kutoka mkoani Mtwara inatarajia kusafiri kuja jijini Dar es Salaam kuivaa timu ya Simba siku ya jumamosi huku ikitanba kushinda katika mchezo huo. https://youtu.be/UX5iASdbTT4

SIMU.TV:  Bingwa wa mbio za mita 3000 na kuruka viunzi kutoka Kenya Ezekieli Kimboi aliyeshinda nishani ya shaba amenyang’anywa nishani hiyo baada ya Ufaransa kukata rufaa ya ushindi wake. https://youtu.be/1_5Kngkn1tw

SIMU.TV:  Chama cha mpira wa miguu wilayani Manyoni mkoani Singida MADIFA kinafanya maandalizi ya kufanya uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu za chama hicho.https://youtu.be/hBpmTx76Qdk

SIMU.TV:  Mchezaji Ryad Mahrez amesaini mkataba na klabu yake ya Leicester city na kukata mzizi wa fitina wakudhaniwa kuwa ataondoka katika klabu hiyo.https://youtu.be/J8dteeQZq_s

KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...