SIMU.TV: Serikali ya Tanzania imesema imeanza mchakato wa kushirikisha wananchi kuchangia maoni yao juu ya kubadilisha kwa sheria ya ndoa ya sasa inayoonekana kuwa kandamizi kwa wanawake; https://youtu.be/3rIwDf-689o

SIMU.TV: Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof Makame Mbarawa, ametoa siku 14 kwa mkandarasi anayejenga barabara wilayani Sumbawanga kurudisha vifaa na kuendelea na kazi; https://youtu.be/cR41cwg4Lbo

SIMU.TV: Wakazi wa wilaya ya Igunga mkoani Tabora, wamemshukuru Rais Magufuli kwa kutoa agizo la kuanza kufanya kazi kwa soko lao; https://youtu.be/thcK5duLqRI

SIMU.TV: Waziri wa Maliasili na utalii Prof Jumanne Maghembe, amezindua bodi ya wakurugenzi ya bodi ya utalii nchini na kuitaka bodi hiyo kuongeza idadi ya watalii;https://youtu.be/EnYfivzMBOs 

SIMU.TV: Shirika la umoja wa mataifa lam maendeleo na bisahara UNCTAD, limeuingiza mkoa wa Njombe katika mafunzo ya kufuga ng’ombe kitaalamu;https://youtu.be/qT9T_lYcSnE

SIMU.TV: Serikali ya mkoa wa Dar es Salaam imetoa agizo kwa watu wote waliovamia maeneo ya wazi waondoke mara moja kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.https://youtu.be/4rXX6j9lS-Q

SIMU.TV: Waziri wa katiba na sheria Dr. Haryson Mwakyembe amesema serikali imefanya jitihada kubwa za kuhakikisha inalinda uhuru na haki za mwanamke.https://youtu.be/3oX9dpXzccw

SIMU.TV: Serikali imepiga marufuku tabia ya wananchi kutumia vyandarua wanavyogaiwa kufugia kuku au kuvitumia kupandia miti. https://youtu.be/-5bNXAx2Pc4

SIMU.TV: Jumla ya hati laki tatu zinatanatarajiwa kutolewa kwa wakazi wa Dar es Salaam baada ya zoezi la urasimishaji wa makazi holela kukamilika. https://youtu.be/OX0c-GC84Yw

SIMU.TV: Jumla ya watu 93 kati ya watu 1453 waliojitokeza kuchangia damu katika mkoa wa Tanga wamebainika kuwa na homa ya ini. https://youtu.be/xPQIb_-d7PY

SIMU.TV: Wachinjaji wa ng’ombe na mbuzi katika machinjio ya Vingunguti jijini Dar es Salaam wamegoma kufanya kazi kutokana na kupandishiwa ushuru.https://youtu.be/M_V8l5eUsXg

SIMU.TV: Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu imesogeza mbele kesi inayomkabili  mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antipas Lisu ya kutoa maneno ya uchochezi.https://youtu.be/1cpA8TL8YJY

SIMU.TV: Serikali imepiga marufuku kilimo cha mkataba kilichokuwa kikimnyonya mkulima kutokana na mnunuzi kujipangia bei ya mazao. https://youtu.be/uihwW2qN_NU

SIMU.TV: Serikali imeishauri mifuko ya hifadhi za jamii hapa nchini kutumia huduma za utuzaji wa dhamana za uwekezaji ili kuwezesha fedha za wateja wao kuwa salama zaidi.https://youtu.be/ukt9omDKAhs

SIMU.TV: Baadhi ya taasisi za fedha zimeanza kuitikia wito wa serikali wa kushusha riba za mikopo ili kuwapa fursa watanzania wengi kupata mikopo.https://youtu.be/yQZXb5osMUE

SIMU.TV: Shirikisho la mpira wa miguu TFF limesema halitatoa leseni kwa mchezaji ambaye timu yake haikuwasilisha mkataba wake kwa TFF. https://youtu.be/d8gFwFIfYwU

SIMU.TV: Mwanachama wa klabu ya Simba Mohamed Dewj ameikabidhi klabu hiyo kiasi cha shilingi milioni mia kwa ajili ya usajili wa wachezaji. https://youtu.be/JUJ3oCO9Zv4

SIMU.TV: Takribani wasanii 10 wa filamu na muziki nchini wanatarajia kunufaika kwa kujiingizia kipato kupitia mitandao ya kijamii kufuatia kuanzishwa kwa b nary itakayosimamia urushwaji wa matangazo kwa mitandao yote ya kijamii.https://youtu.be/99gmONc9-vE

SIMU.TV: Wanafunzi wa kike wametakiwa kutojiweka kando bali washiriki katika michezo ili kuweza kuonesha vipaji vyao na kuviendeleza. https://youtu.be/hLY42CzFuw4

SIMU.TV: Manchester city imekamilisha usajili wa kiungo chipukizi Leroy kwa kiasi cha pound milioni 35 akitokea Schalke 04. https://youtu.be/Ap9iBI5jMhY

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...