SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza kua waalimu wote wanatarajia kusafiri bure kwenye usafiri wa treni ya abiri jijini Dar es salaam.https://youtu.be/uuHgPBv1-cU
SIMU.TV: Taasisi ya sayansi na teknolojia ya Nelson Mandela inatarajia kuanza mradi wa kusafisha maji ya bwawa la Nadosaito wilayani Monduli ili wananchi wapate maji safi.https://youtu.be/jiqNgrflcxw
SIMU.TV: Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imetengua uamuzi uliotolewa na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu wa kufuta kosa la utakatishaji wa fedha kwenye kesi ya Hary Kitilya na wenzake. https://youtu.be/zB2tU_YAJbs
SIMU.TV: Baadhi ya shule mkoani Manyara zinaelezwa kukabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa hali inayowafanya wanafunzi kusomea kwenye bweni katika shule ya sekondari Engeno wilayani Simanjiro. https://youtu.be/-QEutPcpC84
SIMU.TV: Moto umeteketeza baa maarufu ya Carebean iliopo eneo la Sinza jijini Dar es Salaam na kusababisha uharibifu mkubwa. https://youtu.be/mLm4JR740zA
SIMU.TV: Shule ya msingi Msufini iliopo Mbagala jijini Dar es Salaam inakabiliwa na upungufu mkubwa wa madarasa kutokana na kuwa na wanafunzi wengi.https://youtu.be/qxC_K5GadzM
SIMU.TV: Uongozi wa bodi ya utalii nchini TTB umetembelea kampuni ya habari ya Africa Media Group ili kuangalia namna ya kushirikiana katika kukuza utalii wa ndani.https://youtu.be/maeWbvvau0s
SIMU.TV: Shirika la viwango nchini TBS limeanza mazungumzo ya uboreshaji wa matakwa ya viwango na wadau ili kuwa na bidhaa zenye viwango vinavyokubalika.https://youtu.be/mqf7_v5hyz0
SIMU.TV: TBS imekifunga kiwanda cha uzalishaji wa mikate cha Herry Bakery kutokana na kuzalisha bidhaa bila kuwa na nembo ya ubora. https://youtu.be/4D3lL1jx-jY
SIMU.TV: Ligi ya taifa ya mpira wa wavu inatarajiwa kuanza tarehe kumi na nane mwezi huu wilayani Kibaha mkoani Pwani na itashirikisha timu kutoka mikoa mbalimbali.https://youtu.be/jb61SteedIE
SIMU.TV: Mashindano ya michezo mbalimbali yaliyoandaliwa na mbunge wa jimbo la Songea mjini yamehitimishwa kwa washindi kukabidhiwa zawadi zao.https://youtu.be/rYO_tKZOXF8
SIMU.TV: Meneja wa klabu ya Arsenal amesema hatma yake ya kuendelea kuifundisha klabu hiyo itategemea matokeo ya klabu hiyo msimu huu wa ligi kuu Uingereza.https://youtu.be/d6DNxIjl74w
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...