SIMU.TV: Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amesema licha ya kuwepo kwa sheria lakini vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto wa kike vimekithiri nchini. https://youtu.be/NjrB1UaXRUM

SIMU.TV: Rais John Magufuli leo amemuapisha Mrisho Mashaka Gambo kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha na kuchukua nafasi ya Felix Ntibenda ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.https://youtu.be/93X7SsrJDsA

SIMU.TV: Rais Dr John Pombe Magufuli leo amekutana na rais mstaafu wa benki ya maendeleo Afrika AfDB na kumshukuru kwa mchango wake alioutoa kwa nchi wakati akiwa rais wa AfDB. https://youtu.be/xU7Uhmlvpvo

SIMU.TV: Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu leo imetupilia mbali ombi la upande wa jamhuri linalomtaka wakili Peter Kibatala kutomtetea Tundu Lisu kwa madai kuwa sheria hairuhusu shahidi kuwa mtetezi. https://youtu.be/yYtl2Gn8TC0

SIMU.TV: Serikali mkoani Kilimanjaro imewatahadharisha wakazi wanaoishi kuzunguka bwawa la Nyumba ya Mungu kujitahadharisha na uvuvi haramu.https://youtu.be/KgKrkvs1_QQ

SIMU.TV: Wenyeviti wa mitaa kutoka manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam wamekusanyika katika ofisi za manispaa hiyo kudai malipo ya posho zao. https://youtu.be/9PzD60n6FW8

SIMU.TV: Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kupitia kitengo chake cha Vodacom foundation imetoa msaada kwa shirika la Tumaini ya maisha ili kusadia mpango wa lishe kwa watoto wenye saratani. https://youtu.be/mcVs-bJXU-M

SIMU.TV: Tanzania inatarajia kutumia tukio la kupatwa kwa jua Septemba mosi mwaka huu kuvitangaza vivutio vya utaalii vinavyopatikana nchini.https://youtu.be/VBGLydUXwrA

SIMU.TV: Kampuni ya utengenezaji wa magari ya Nissan imesema imejipanga kuzingatia sheria za uwekezaji nchini ili kuwezesha maendeleo ya uchumi. https://youtu.be/Q-Nuq9PBvU0

SIMU.TV: Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajia kuanza hapo kesho huku timu ya Simba ikitarajia kufungua mzunguko wake na timu ya Ndanda kutoka Mtwara.https://youtu.be/p2Zy5cXs5H0

SIMU.TV: Shirikisho la soka Tanzania TFF limemthibisha mchezaji Hassan Kessy kuichezea klabu ya Yanga huku akitakiwa kuilipa klabu ya Simba. https://youtu.be/gr_eQAS4B1Q

SIMU.TV: Mchezaji mkongwe wa zamani wa Taifa na timu ya Maji maji Kelvin Haule amefariki dunia katika hospitali ya rufaa ya Songea alipokuwa akipatiwa matibabu.https://youtu.be/x2yTjvdnmg4

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...