Hasa
kwa wale wanaonunua magari kwa mara ya kwanza, na hawana uzoefu wa
kuendesha gari, na pia wale wote ambao wanaweza wakawa wana uzoefu wa
kuendesha gari mijini, lakini hawana uzoefu wa kuendesha gari kwenye
bara bara kuu za kwenda mikoani.
Lakini ni vema kila mtu aliye dereva akasoma ninachoeleza hapa. Inaweza
kuokoa maisha yako ya familia yako, na wengine wanaoendesha magari au
kuwa abiria.
Ndugu
zangu, ukiweza kuendasha gari hapa Dar, au hata mikoani mijini, haina
maana utaweza kuendesha gari pasipo tatizo kwenye barabara kuu.
Nimeshuhudia watu wengi sana waliokufa kwa sababu baada ya kununua gari
walikuwa na mchecheto wa ku-drive kwenda kwao kijijini.
Kuendesha gari kwenye barabara kuu ni tofauti sana na kuendesha gari
mijini. Kwenye barabara kuu challenge zake ni kubwa sana kwa sababu gari
zinaenda kwa kasi, na pia kuna mambo mengi ya ghafla yanayoweza
kujitokeza ambayo kama huna uamuzi wa haraka kama dereva utakufa tu
kabla ya kufika mwisho wa safari yako.
Ukifanya
kosa hata dogo barabara kuu unaweza kufa, tofauti na mijini.
Kwa mfano, ku-overtake katika barabara kuu ni jambo linatakiwa lifanywe
kwa makini sana. Na pia kila unapoingia kona kali au blind spot kwenye
barabara kuu weka akilini kwamba unaweza kukutana na kitu upande wako,
basi linaloenda kasi, lori au trekta liloharibika, mifugo, shimo kubwa,
mawe yaliyoporomoka, ajali nk. Pia unaweza kukutana ghafla na dereva
mzembe anae-overtake kwenye kona na yuko upande wako.
Usithubutu ku-overtake sehemu ambayo huoni mbali mbele, na usikaribie
sana gari unayotaka ku-overtake kabla ya kui-overtake. Na unapo-overtake
kama una gari manual gear, rudi gia za chini kwanza ili kujenga spidi
ya ku-overtake.
Kama
una gari automatiki, ikibidi itoe gari kwenye overdrive (unabonyeza
kiswitch cha Overdrive na kuna kataa katawaka kwenye dashboard kuonyesha
Overdrive iko off), hasa kama ulikuwa umepunguza mwendo. Mara nyingine
toa gia kwenye "D" na rudi kwenye "2" ili kujenga spidi ya ku-overtake,
na ukishamaliza rudi kwenye D na Overdrive. Hili ni muhimu sana kwa gari
ambazo ukikanyaga accerator gari inakawia kuchanganya.
Overtake
kwa haraka, sehemu ambayo iko salama, na ni vizuri gari unayoi-overtake
dereva wake ajue unamu-overtake. Unaweza kumpigia honi kidogo ya kuibia
kama kuomba - usipige kwa nguvu ukamuudhi. Epuka kuovertake sehemu ya
barabara yenye mashimo, maana dereva wa mbele anaweza kurudi upande wako
ili akwepe shimo wakati tayari unamu-overtake.
Siri moja ya ku-overtake salama ni uvumilivu - overtake nzuri haitaki
haraka.
Na
pia kosa linaloua watu wengi sana ni ku-overtake kwa kukisia kwamba
hakutakuwa na gari inayokuja upande wa pili zile sehemu ambazo huoni
vizuri mbele. Hata kama barabara haina magari mengi usithubutu kukisia
kwamba hakutakuwa na gari (gambling overtake).
Na pia katika barabara kuu kuna suala la uchovu - fatigue. Hili ni jambo
jingine linaua sana watu wasio na uzoefu wa kuwa katika barabara kuu.
Ni mbaya hata zaidi ikiwa utakaposimama mahali kwa chakula ukanywa bia -
hata moja tu, kwa sababu itakuletea sana usingizi.
Epuka
kula vyakula vizito kama ugali na maharage, au kula hadi ukashiba sana!
Ukisikia usingizi simama upumzike, toka ndani ya gari, tembea kidogo,
kabla ya kuendelea na safari. Kama ikibidi tumia Redbull (sio zaidi ya moja).
Na
jambo jingine muhimu sana la kukumbuka ni kwamba ukiingia barabara kuu,
ukaendesha kwa muda fulani, akili yako inazoea spidi kali kiasi kwamba
huoni tena kama unaenda spidi kali. Unaweza ukawa unaenda 140km/h ukaona
kama unaenda 80km/hr.
Hili
huwa mara nyingi linasababisha kuacha njia na kupinduka, au kuingia
kona ukiwa na spidi kubwa na gari kupinduka. Nadhani umesikia sana ajali
zinazosemwa zilitokea kwa sababu dereva alishindwa kumiliki gari - ni
kwa sababu akilini dereva aliona haendi spidi.
Na
pia jambo jingine muhimu sana kukumbuka ni kwamba, unapoenda safari
yoyote ya mbali ambayo utaendesha gari mfululizo kwa zaidi ya masaa
manne, au kwa spidi zaidi ya 100km/hr, hakikisha tairi zako hazina umri
zaidi ya miaka mitano, la sivyo utapata basti hata kama tairi inaonekana
bado mpya kwa
kuitazama. Tairi ikizidi miaka mitano haifai kusafiria safari ya mbali,
japo unaweza ukaendelea kuitumia kwa safari za mijini.
Nimeona niseme haya kwa sababu nawapenda ndugu zangu.
Sitaki
mufe barabarani, au mniue mie na familia yangu. Wapeni taarifa wengine
ili tuzidi kuepuka vifo hivi vya barabarani ambavyo vingi vinazuilika.
Neno langu la mwisho, ili uendeleee kuwa salama barabarani ni kwa lugha
ya kiingereza; BE PATIENT kwa lolote unalotaka kufanya ukiwa unaendesha
gari. Zingaitia hilo, utakuwa salama.
umefafanua vizuri, ila kazi ya overdrive sijaipata vizuri. is it for quick accelerating or what. what does it do
ReplyDeleteThanks. Very educative. Be blessed!
ReplyDeleteSafi sana haya ndio ya kuandika . sio habari za ukuta ukuta kila kukicha na za kina wacheza viduku. Big up mkuu
ReplyDelete