Na Mwene Saidi
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa madai ya kutoa lugha ya uchochezi na kwamba mapema kesho anatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Akizungumza na Blogu ya Jamii kwa njia ya simu ,Wakili wa Lissu, Peter Kibatala alisema mteja wake alikamatwa jana mkoani Singida.
"Alikamatwa jana saa 12 jioni mkoani Singida wakaanza safari akiwa chini ya ulinzi hadi Kituo cha Polisi Chamwino Mkoani Dodoma

"Leo mchana waliwasili Kituo Kikuu Cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam...walianza kumhoji saa 9 hadi 9;30 Mahojiano yalihusu kujihusisha na matamshi ya uchochezi katika viwanja vya mahakama ya Kisutu" alisema Kibatala.
Aidha alisema kwa mujibu wa sheria hadi kufika kesho asubhi Lissu atakuwa amekaa chini ya ulinzi wa polisi kwa masaa 36 kwa hiyo inatakiwa apelekwe mahakamani ama kuachiwa kwa dhamana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...