Ukosefu wa maarifa na taarifa sahihi wa vipindi vya mabadiliko maisha ya vijana husababisha uwezekano wa kupotoka kimaadili kwa kufanya mafunzo kwa vitendo na kuathiri makuzi bora.

Akitoa mafunzo kwa wanafunzi wanaounda vikundi vya kutayarisha vipindi vya redio kwa ajili kupaza sauti zao kuieleza Jamii kuhusu hali zao mashuleni, mamlaka mbalimbali, majumbani na katika Jamii wilayani Sengerema na Pangani, Afisa Mtaalam masuala ya Afya wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Herman Mathias alisema kwamba changamoto nyingi zinazoathiri makuzi ya kimaadili kwa vijana ni kutopewa maarifa na taarifa sahihi jinsi ya kutumia miili yao bila kuathiri ndoto zao.

“Vijana wengi wameshindwa kufikia ndoto zao kutokana na kutomaliza shule kwa sababu hawajui namna ya kufanya maamuzi sahihi kutumia fursa walizo nazo”, alisema Herman Mathias.

Mwezeshaji Herman Mathias kutoka UNESCO akitoa somo kwa washiriki wa Shule za Sekondari Sengerema.

Ili kufikia malengo ya ndoto zao Afisa huyo wa UNESCO alisema vijana wanahitaji kusoma kwa bidii na kuhitimisha mzunguko wa elimu, kuwa na tabia njema kwa kuepuka vishawishi vya mtaani hususan kuvuta bangi na matumizi ya vileo, utoro na matumizi ya lugha mbaya.

Alizitaja tabia njema nyingine pamoja na kuepuka tabia za kimapenzi yanayoweza kusababisha magonjwa ya zinaa, maambikizi ya virusi vya UKIMWI na ujauzito na upatikanaji wa malezi yanayojali nafasi na muda wa mtoto na kuweka mazingira rafiki ya kuishi na kusoma, afya bora kwa kutougua hovyo magonjwa mbalimbali na kuwa msafi wakati wote hali inayompa fursa kijana kushiri katika shughuli zote za kijamii na kielimu na kuwataka wazazi na walezi kufuatilia mwenendo wa kijana shuleni na katika Jamii.

Zaidi ya asilimia 52 ya vijana hawana elimu ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI na afya ya uzazi.

Alisema kwamba mambo hayo yote yanawezekana kuepukika kwa sababu yako ndani ya uwezo wa vijana wenyewe na wazazi pia.
Washiriki wakichangia mawazo na uzoefu wao kuhusu changamoto zinazowakabili.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...