Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limepiga marufuku
maandamano ya Chama cha Demokrasia Maendeleo (CHADEMA) yanayopangwa
kufanyika Septemba 1 mwaka huu. Maandamano hayo yamepewa jina
la UKUTA ambapo wanachama wake wanataka kuingia mitaani kupinga kile wanachokiita ukandamizaji wa demokrasia.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya
Dar es Salaam, Simon Sirro amesema leo kwamba maandamano hayo hayatafanyika na jeshi la
polisi limejipanga kuzuia maandamano hayo.
Kamanda Sirro amesema kuwa hakuna habari ya Ukuta na hakuna mtu
atakayedhubutu kuingia barabarani kutokana jeshi lilivyojipanga kuhakikisha
wananchi wanafanya shughuli zao bila kuingiliwa na kitu chochote.
Amesema kuwa utaratibu wa kufanya mikutano ya siasa umeelezwa
hivyo kufanya mikutano bila kufuata utaratibu hautaruhusiwa.
Kamishina Sirro amesema kuwa kikundi/watu wanaotaka
kutumia siasa katika kuvunja Amani kwa Dar es Salaam hakuna kitu chochote
kitafanyika kutokana na jeshi la polisi lilivyojipanga.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es
Salaam, Agasti 20 majira ya saa 12:00 jioni lilipata taarifa toka kwa raia wema
kuwa maeneo ya mtaa wa Ufipa Kinondoni kuna duka linauza flana rangi mbalimbali
zenye maneno ya uchochezi yaliyoandikwa ‘’TUJIPANGE TUKATAE UDIKITETA UCHWARA’’
rangi nyeupe idadi yake 28, rangi nyekundu fulana 18 zenye maneno ‘UKUTA’
fulana 6 za Kakhi zenye maneno ‘’UKUTA’ Na fulana
zingine rangi nyeusi 23 zenye maneno ’’UKUTA’’.
Aidha Polisi baada ya kupata taarifa
hizo walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa Yoram Sethy Mbyelllah (42)
mfanyabiashara, mkazi wa Mburahati akiwa anauza fulana hizo dukani kwake.
Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na baada ya upelelezi kukamilika atafikishwa
mahakamani.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akizungumza na waandishi habari juu ya Operesheni mbalimbali za kanda hiyo pamoja na kuzuia maandamano ya UKUTA, jijini Dar es Salaam leo.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akionyesha magazine ya kuwekea risasi zilizokamatwa jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akioyesha bastola aina ya Browning yenye risasi sita iliyokamatwa jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akionyesha site Mirror zilizoibwa katika magari leo jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akionyesha flana rangi mbalimbali zilizokamatwa.
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...