Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amefungua rasmi mashindano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya na kuvitaka vilabu vya soka kutumia vipaji vinavyoibuliwa na programu hiyo ya vijana. Ufunguzi huo ulifanyika kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya leo Agosti 9, 2016.

“Hii ndio njia pekee ambayo inaweza kutuletea maendeelo ya soka na kuiwezesha nchi yetu kuondokana na matokeo mabaya katika mashindano mbali mbali ya kimataifa”, alisema. Aliishukuru kampuni ya Airtel Tanzania kwa kubuni programu hii ambayo imekuwa ikiwapa vijana fursa ya kuonyesha na kuviendeleza vipaji vyao.

Makala amewataka vijana kucheza kwa kujituma na kufahamu kwamba hatma ya mchezo wa soka hapa nchini iko mikononi mwao. Alilitaka Shirikisho la soka nchini (TFF) kufanya kazi kwa karibu na wadau wengine ili kuhakikisha kuwa vijana wanaoibuliwa kupitia Airtel Rising Stars wanaendelezwa.

Amewataka viongozi wa chama cha soka mkoa wa Mbeya (MREFA) kuyatumia vizuri mashindano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa na kuchagua vijana nyota watakaounda timu za mkoa kushiriki kwenye fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Septemba 6 hadi 11 jijini Dar es Salaam.

Michuano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa inaendelea katika mikoa minginge ambapo timu za wavulana za Makongo Sekondari na Kawe United zilitoshana nguvu baada ya kutoka suluhu katika uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Fainali za Taifa zitashirikisha timu za wavulana na wasichana kutoka mikoa ya kisoka ya Ilala, Temeke na Kinondoni. Timu nyingine zitatoka Morogoro, Mwanza, Mbeya, Arusha, Lindi na Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amoss Makalla aliye simama akizungumza na wachezaji kabla ya kuzindua michuano ya Airtel Rising Star kwa Mkoa wa Mbeya iliyo anza kutumia vumba jana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kushirikisha timu sita.
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mbeya wakati wa uzinduzi wa michuano ya Airtel Rising Stars mkoani hapo
Wachezaji kutoka timu sita zinazo shiriki Michuano ya Airtel Rising Star chini ya miaka 17 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amsos Makalla hayupo katika picha kabla ya kuzindua rasmi michuano hiyo kimkoa jana katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...