Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Mhandisi
Steven Mlote(kushoto)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo jijini
Dar es Salaam,wakati wa alipokuwa akitoa tamko la baraza hilo juu ya
kuvifutia Usajili baadhi ya vyuo ambapo kati ya 175 vimepewa notisi ya
kushushwa hadhi na 5 vimefutiwa Usajili na 41 vimetakiwa kujisajili mara
moja ,ikiwa katika jitihada za kuboresha elimu ya ufundi nchini,Katikati
Kaimu wa baraza hilo Dkt. Adolf Rutayuga na Mkurugenzi wa
Udhibiti,Ufuatiliaji na Tathimini Bi. Agness Ponera.
Baadhi ya wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
wakiwa kwenye mkutano wakati Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhandisi
Steven Mlote(hayupo pichani)alipokuwa akiongea na waandishi habari jijini
Dar es Salaam kuhusiana na tamko la baraza hilo kuvifutia Usajili baadhi
ya vyuo ambapo kati hivyo 175 vimepewa notisi ya kushushwa hadhi na 5
vimefutiwa Usajili na 41 vimetakiwa kujisajili mara moja,ikiwa katika jitihada
za kuboresha elimu ya ufundi nchini.
Baraza la Taifa la Elimu ya
Ufundi (NACTE) limetangaza kuwa vyuo 5
vimefungwa kuendesha mafunzo na kufutwa kwenye rejista ya vyuo vya ufundi
nchini.
Pia Baraza limetangaza kuwa vyuo
41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria vimepewa
muda wa wiki mbili na kutakiwa vijisajili mara moja kwenye Baraza hilo kabla ya
kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Vilevile, vibali vya usajili wa vyuo 112 vya kutoa elimu ya ufundi
vimefikia ukomo hivyo vinapaswa kutekeleza masharti ya Usajili; wakati vyuo 57 vimefikia ukomo wa ithibati, hivyo
inapaswa kutekeleza masharti ya ithibati, imetangazwa jana.
Akiongea katika mkutano na
waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Baraza (NACTE), Mhandisi Steven Mlote,
amesema Baraza limetoa muda wa mwezi mmoja kwa vyuo 112 kutekeleza masharti ya
usajili na vyuo 52 kutekeleza masharti ya ithibati kwa mujibu wa sheria za
uendeshaji vyuo vya ufundi nchini, na vyuo vitakavyoshindwa kutekeleza agizo
hili vitafungiwa mara moja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...