Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
VYAMA vinne vyenye uwakilishi bungeni vimesema kuwa watarejea bunge lijalo kutokana na ushauri wa viongozi wa dini waliokaa kujadili sintofahamu kwa vyama hivyo.

 Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia amesema viongozi wa dini wamefanya kazi kubwa katika majadiliano hayo kwa kuweka masilahi mapana ya taifa.

Amesema kuwa kurudi katika bunge lijalo mpaka wabunge wote wa vyama wakutane na kuweza kufikia mwafaka huo kutokana na ushauri wa viongozi hao.

Mbatia amesema kuwa kuna vitu vingine huwezi kuangalia katika katiba huvyo unahitaji busara zaidi kwa kuangalia masilahi mpana ya taifa.

Amesema kuwa NaibuSpika , Dk.Tulia Ackson anatakiwa kuweka busara katika kuongoza bunge na kuacha taratibu kanuni za bunge pamoja na katiba.

Aidha amesema kuwa viongozi wa dini wameshauri vyama kurejea bungeni na kutaka masuala yao wanayoyataka kikatiba yatatuliwe.
 Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya vyama vinne vyenye uwakilishi bungeni  vitarejea bunge lijalo kutokana na ushauri wa viongozi wa dini waliokaa kujadili sintofahamu kwa vyama hivyo katika mkutano uliofanyika leo Makao Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zanzibar, Said Issa Mohamed akizungumza na waandishi habari juu ya maazimio ya viongozi wa dini jana katika mkutano uliofanyika leo Makao Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI.
Waandishi wakimsikiliza Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia leo Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Face saving and an expression of sheer foolishness. Did they truly had to wait for devine intervention? They could easily have walked from the parliament to their respective houses of worship for guidance. What a gang of empty heads.

    ReplyDelete
  2. Hao viongozi wa dini wamewaambia kipi ambacho wao wenyewe walishindwa kukifikiria. Labda viongozi wa dini wachukue nafasi zao Bungeni. Anachosema Mbatia hata hakina mwanga wowote. Wamechanganyikiwa. Hivi kweli hawa ndio viongozi wetu Bungeni? Mungu Ibariki Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...