Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa Maiko Lekule Laiser ,akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Daud Filex Ntibenda, aliyepo kushoto kwa mkuu huyo ni mwenyekiti wa Taso kanda ya Kaskazini ndugu Athar Kitonga Shayo wakiwa katika uzinduzi wa maonyeho hayo ya wakulima na wafugaji katika viwanja vya Taso Themi nanenane Njiro Jijini Arusha.


Na Woinde Shizza,Arusha

Mkuu wa mkoa wa Arusha Daud Filex Ntibenda amewataka Wakurugenzi wote wa Mikoa yote mitatu iliyopo Kanda ya Kaskazini ,wabadilishe mabanda yao na wajenge ya kisasa zaidi kwaajili ya maonyesho ya wakulima na wafugaji ambayo yatakuwa na mvuto zaidi.

Aliyasema hayo alipokuwa kifungua maonyesho ya nanenane yanayoendelea katika viwanja vyaThemi nanenane Njiro Jijini Arusha,huku akiwataka Taso washirikiane na Jiji pamoja na viongozi wa mikoa yote ili waweze kutengeneza ukumbi mkubwa wa kisasa.

Aidha alisema kumekuwa na changamotoya wananchi.kutoielewa kauli mbiu ya maonyesho ya nanenane mwaka huu hivyo basi amewaagiza wakulima na wafugaji waweze kuingia.kwenye mafunzo ya shamba darasa na kwenye mabanda ili waweze kupata elimu zaidi.

Aliwaagiza washiriki wenye mabanda yenye technolojia za kilimo waandae taarifa fupi ambayo mwananchi atakwenda nayo nyumbani na zitakazo waletea mabadiliko katika maeneo wanayotokea.

Sambamba na hayo aliwataka Taso kuangalia sheria viwanja vya maonyesho ambayo inapiga marufuku ongezeko la makazi ndani ya viwanja vya maonyesho,pia amewataka washiriki wote wa maonyesho watoe ushirikiano kwa vyombo vyabulinzi na Usalama na katika maeneo yao.

Vijana wa JKT Oljoro wakiwa wanatoa burudani siku ya uzinduzi wa maonyesho ya wakulima na wafugai ya nayandelea katika vianja vya Taso Themi nanenane mi njiro Arusha.
Meya wa Jiji la.Arusha wa pili kutoka kulia ndugu Calist Lazaro a
kiteta jambo na diwani wa kata ya Themi Melance .E.Kinabo wa kwanza kulia katika maonyesho yanayoendelea katika maonysho yanayoendelea katika viwanja vya Taso nanenane Njiro Jijini Arusha.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mrisho Gambo akiwa anatoa utambulisho.kwa.viongozi mbalimbali waliohudhuria sikubyaufunguzi wa.maonusho ya wakulima na wafugaji yanayondelea katika viwanja vya Themi Njiro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...