Mbunge wa jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega amezindua kisima cha Maji katika kijiji cha Mwalusembe ambacho kimejengwa katika shule ya msingi muongozo Kwa ufadhili wa Taasisi ya Afraca Reflection Foundation
Mara baada ya uzinduzi huo Ulega aliwashukuru wafadhili hao nakuwaomba kuendelea kusaidia wilaya hiyo ili kukabiliana na uhaba wa Maji uliopo na kwamba Mkuranga ni moja ya maeneo ambayo yanachangamoto kubwa ya Maji....Pia aliwataka wananchi wa kijiji hicho kutumia Maji hayo vizuri ikiwa pamoja na kulinda miundombinu Yake ikiwamo solar na vinginevyo ili visiibiwe...ulega tangu kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge wa jimbo hilo tayari ameshachimba visima katika vijiji zaidi ya vitano huku akisaidia kutatua mambo mbalimbali ambayo yamekuwa kero Kwa watu wake.
Mbunge wa jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizindua kisima cha Maji katika kijiji cha Mwalusembe ambacho kimejengwa katika shule ya msingi Mwongozo Kwa ufadhili wa Taasisi ya Afraca Reflection Foundation leo mkoani Pwani.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga,Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwalusembe kweye hafla ya uziduzi wa kisima cha Maji katika kijiji cha Mwalusembe ambacho kimejengwa katika shule ya msingi Muongozo kwa ufadhili wa Taasisi ya Afraca Reflection Foundation mkoani Pwani.
Mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega katika kijiji cha Mwalusembe kwa ajili ya kuziduzi kisima cha Maji ambacho kimejengwa katika shule ya msingi Muongozo mkoani Mpwani. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...