Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Old East International Moses Mwano akiwa anazungumza na wateja waliotembelea banda hilo katika Maonyesho yanayoendelea katika Viwanja vya Taso nanenane Njiro Jijini Arusha.
Meneja mauzo wa Kampuni Old East International akiwa anamfafanulia mteja juu ya Crown Cartridge,katika maonyesho yanayoendelea katika viwanja vya Taso nanenane.
Afisa Mipango wa Kampuni Old East International Ephrahim Moses Mwano akiwa anaonyesha Aina ya Wino wa Crown ambao wanatengeneza hapa nchini,Katika maonyesho ya wakulima na wafugaji Katika viwanja vya nanenane Njiro Jijini Arusha.

Na Woinde Shizza,Arusha.
Wito umetolewa kwa Watanzania watumie na kuthamini bidhaa zinazotengenezwa na kupatikana ndani ya nchi badala ya kuzipa kipaumbele bidhaa za nje ya nchi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Old East International ndugu Moses Mwano ,katika maonyesho yanayoendelea katika viwanja vya Taso nanenane njiro Jijini Arusha.

Mwao amesema kuwa Watanzania wengi wanathamini bidhaa zinazoingia nchini kutoka nje ya nchi,ambazo baadhi hazina kiwango cha ubora unaotakiwa kwa mtumiaji.

Mkurugenzi huyo wa Kampuni ya Old East International amesema kuwa kampuni hiyo ni ya Kitanzania ,imesajiliwa na ipo chini ya Shirika la uwekezaji Tanzania wao ni wawekezaji wa ndani,wanahusika kutengeneza wino wa kuchapia unaofahamika kwa jina la Crown Cartridge.

Kwa upande wake Mwano amewataka Watanzania kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dokta John Magufuli,katika jitihada zake za kuifanya Nchi kuwa ya Viwanda.

Sambamba na hayo amewaasa Watanzania watengeneze na kuingiza Bidhaa zenye kukidhi ubora na viwango ,huku akimalizia na msemo usemao " kizuri cha jiuza kibaya chajitembeza akimaanisha kuwa ukitengeneza bidhaa nzuri yenye kukidhi viwango na ubora unaohitajika wateja watafurahiwa nayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...