Waziri wa Wizara ya  Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi Akizungumza na Maafisa mipango miji jijini Dar es salaam leo. Kulia Mkurugenzi wa Nyumba wa Wizara ya  Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Michael Mwalukasa.
Baadhi ya waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Wizara ya  Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumza na maafisa wa mipango miji.

WAZIRI wa Wizara ya  Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewataka wawekezaji wa ndani na nje ya nchi (Real Estae Developers) kujenga nyumba bora mkoani Dodoma.

Akizungumza na maafisa wamipango miji jijini Dar es salaam leo Waziri Lukuvi amewataka watendaji hao kuweza kujipanga kujenga nyumba za makazi  za watumishi wa Serikali ilikuweza kuwahudumia watumishi hao wanaotarajia kuhamia mjini Dodoma.

''Lengo la kikao hiki ni kuwataka mjipange ili kuweza kujipanga ni namna gani mtaweza kuhudumia watumishi wa serikali wakati wakiwa mjini Dodoma''amesema Waziri Lukuvi.

Amesema kuwa sambamba na wizara mbalimbali kuhamia katika jiji la Dodoma amewataka watendaji hao kuweza kuboresha ramani ya mipango miji ilikuonesha namna gani mji unavyotakiwa kukaa ikiwemo kuboresha miundombinu ya majengo .

''Tumeshamaliza mastar Plan tangu mwaka 2010 ya Dodoma kwani maeneo mengi yakuishi yameshaainishwa nilazima maafisa mipango kufanya biashara ikiwemo viwanja vyandege.


Nae Katibu wa Wizara hiyo, Michaeli Mwalukasa amesema kuwa serikali inaandaa sera ya nyumba ikiwemo muswada wa uendelezaji miliki katika miji mbalimbali hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...