BBALOZI wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida amemtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya nchi zao hususan katika sekta ya nishati.

Balozi Yoshida, aliyeambatana na Ujumbe wa baadhi ya maofisa kutoka Ubalozini na wataalam kadhaa kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC), alimtembelea Prof Muhongo Agosti 3 mwaka huu ofisini kwake, jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida (kushoto) na Mtaalam kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC) la nchini Japan, walipomtembelea Waziri hivi karibuni.
 Kutoka kushoto ni Bwana Hitoshi Suzuki (Ofisa kutoka Ubalozi wa Japan nchini Tanzania), Bibi Sakura Nishioka (Mtaalam kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC), Masaharn Yoshida (Balozi wa Japan nchini Tanzania), Profesa Sospeter Muhongo (Waziri wa Nishati na Madini), Bwana Yoshiaki Igarashi (JOGMEC), Bibi Ayumi Kosug (JOGMEC) na Tamiko Hirata (Ofisa kutoka Ubalozini). Balozi Yoshida na Ujumbe wake walimtembelea Waziri Muhongo ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa tatu kutoka kulia) akizungumza na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida (Kulia kwa Waziri) na Ujumbe wake, walipomtembelea Waziri ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...