Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto) akizungumza na Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uturuki. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kulia) akimsikiliza Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya alipomtembelea ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Viongozi hao walijadili masuala mbalimbali ya kuwahudumia Wakimbizi nchini.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (katikati) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (kushoto) kuhusu masuala mbalimbali ya kuwahudumia Wakimbizi nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi wa Wizara hiyo, Harrison Mseke.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kulia) akimkaribisha ofisini kwake, jijini Dar es Salaam, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya.Viongozi hao walijadiliana masuala mbalimbali jinsi ya kuwahudumia Wakimbizi nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...